Milioni 200 Kutumika Kusambaza Huduma ya Maji Safi wilayani Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, May 07, 2018

Milioni 200 Kutumika Kusambaza Huduma ya Maji Safi wilayani Ngara.

Kikundi cha Ngoma ya Asili cha Wanawake wa CCM Kata ya Rusumo wilayani Ngara mkoani Kagera wakitoa burudani wakati wa mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera  Alex Gashaza Jana May 6,2018.

Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera Mhe. Alex Gashaza amefanya mkutano wa hadhara na Wananchi wa Rusumo katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Kabulanzwili  ambapo alihimiza Miradi mbalimbali ya maendeleo itolewe taarifa na kuwashirikishaViongozi na Wananchi ili itekelezwe kwa ufanisi zaidi.

Ameahidi kuendelea kuizungumzia Bungeni miradi ya maendeleo ambayo bado haijakamilika ikiwemo huduma ya maji safi na salama na wananchi wa Kata ya Rusumo kupewa kipaumbele kwenye mradi wa maporomoko ya Rusumo.

Aidha,Mhe Gashaza,amesema kuwa  wilaya ya Ngara itapatiwa Shilingi Milioni 200 kwa ajili ya Utekelezaji wa mradi wa Maji ambapo zitatumika katika ujenzi wa Matenki mawili makubwa katika mlima Shunga ili kusambaza maji katika wilayani hiyo.

Picha/Habari Na  –Radio Kwizera Ngara.

Wana CCM na Wananchi wakifatilia mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera  Alex Gashaza Jana May 6,2018.




Mbunge wa Jimbo la Ngara mkoani Kagera  Alex Gashaza.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad