![]() |
Walimu waliohamishwa kutoka
shule za sekondari kwenda masingi katika Halmashauri ya mji wa Kasulu mkoani Kigoma,
wameazimia kuendesha mgomo Baridi na kutofika kwenye vituo vyao walivyopangiwa,
mpaka watakapopewa stahiki zao zote
|
![]() |
Walimu hao wameiambia Radio Kwizera kuwa wamefuatilia zaidi ya miezi mitatu sasa tangu kutolewa kwa agizo hilo lakini mpaka sasa hawajapatiwa stahiki zao huku nao wakiahidi kutofika katika vituo walivyopangiwa mpaka stahiki zao zitakapolipwa. |
![]() |
Katibu wa
Chama cha walimu (CWT) wilayani Kasulu Mwl.
Buchumi Felister Nkayamba, amesema msimamo wa chama cha walimu ni kuitaka
halmashauri hiyo kuwalipa walimu stahiki zao kama maelekezo ya Rais
yanavyoelekeza.
Hata hivyo
mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa Kasulu Bi.
Fatina Laayi, alipoulizwa kuhusu malalamiko ya walimu hao amesema hayupo
tayari kulizungumzia suala hilo ambapo radio kwizera inaendelea kufuatilia kwa
ajili ya kupata majib.
|

Na –Radio Kwizera.
No comments:
Post a Comment