Taswira Picha ziara ya Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dkt. Anna P. Makakala wilayani Ngara-Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, September 28, 2017

Taswira Picha ziara ya Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dkt. Anna P. Makakala wilayani Ngara-Kagera.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dr Anna Peter Makakala akiwa wilayani Ngara,mkoani Kagera September 27,2017 .Kushoto kwake ni Mkuu wa wilaya ya Ngara Luten Kanali Michael Mtenjele.

Akiwa wilayani Ngara, Kamishina Jenerali wa Idara ya Uhamiaji Dkt. Anna P. Makakala amewataka wananchi wa Wilaya hiyo kushirikiana na idara ya uhamiaji ili kuwabaini na kudhibiti wahamiaji haramu wanaoingia nchini kupitia vijiji vya Wilaya hiyo.

Pia ameita Kamati  za Ulinzi na Usalama katika wilaya ya Ngara, Misenyi ,Karagwe na Kyerwa mkoani Kagera  kusitisha kupokea wakimbizi katika kambi za muda kwa raia wanaotoka nchi  jirani na  na kwamba nchi wanakotoka wakimbizi hao kuna amani na utulivu hivyo warejee na kujenga nchi yao  kimaendeleo na kiuchumi.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dr Anna Peter Makakala akisalimiana na Watumishi mbalimbali wa Idara ya Uhamiaji  wilayani Ngara wakati wa ziara ya kiutendaji mkoani Kagera September ,2017.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dr Anna Peter Makakala akiwa wilayani Ngara,mkoani Kagera September 27,2017  wakijadiliana Jambo na  Mkuu wa wilaya ya Ngara Luten Kanali Michael Mtenjele kulia.
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dr Anna Peter Makakala kulia akiwa wilayani Ngara,mkoani Kagera wakati wa kikaocha ndani na Watendaji wa Uhamiaji,kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya. kushoto kwake ni  Mkuu wa wilaya ya Ngara Luten Kanali Michael Mtenjele.

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini Dr Anna Peter Makakala akiwa wilayani Ngara,mkoani Kagera ( Katikati) sambamaba na  Viongozi wengine wa Uhamiaji Mkoani Kagera. HABARI ZAIDI BOFYA HAPA KUISOMA.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad