Taswira Picha bora Afrika Wiki hii. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 02, 2017

Taswira Picha bora Afrika Wiki hii.

Katika picha hii iliyotolewa Ijumaa, watoto wanaonekana wakicheza katika Mto Chari katika mji mkuu wa Chad, N'Djamena.

Wafuasi wa kiongozi mkuu wa upinzani Isaias Samakuva, wanaonekana wakuwa na jogoo mweusi, nembo ya chama cha Unita chake Samakuva ambapo katika mji mkuu wa Angola, Luanda, wafuasi wa chama tawala cha MPLA wanaonekana wakiwa na furaha katika mkutano wa kampeni. Mgombea wa chama hicho Joao Lourenco anatarajiwa kuwa rais baada ya Jose Eduardo dos Santos kutangaza atastaafu baada ya kuongoza wka miaka 38.

Katika mji mkuu wa Ghana, Accra, mwanamke huyu alikuwa amevalia mahsusi kuhudhuria Tamasha ya Sanaa ya Barabarani ya Chale Wote.

Mamia ya wasanii wenyeji na kutoka nje ya nchi walihudhuria tamasha hiyo siku ya Jumamosi ambapo waliwatumbuiza waliohudhuria kwa sarakasi, vichekesho, kucheza ngoma na mengine mengi.

Hayo yakijiri, nchini kenya wafuasi wa kiongozi mkuu wa upinzani Raila Odinga waliandamana Nairobi siku ya Ijumaa. Upinzani umewatuhumu polisi kwa kutumia nguvu kupita kiasi kukabiliana na waandamanaji walioandamana kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu wa tarehe 8 Agosti. Polisi wamekanusha tuhuma hizo.

Jumamosi, rais wa Nigeria Muhammadu Buhari, 74, alilakiwa na baadhi ya magavana wa majimbo ya nchi hiyo katika uwanja mkuu wa Abuja baada yake kurejea kutoka Uingereza alikokuwa anapokea matibabu kwa miezi mitatu.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad