Kamanda Sirro: Tumekatata Watuhumiwa 311 wa Dawa za Kulevya. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, February 14, 2017

Kamanda Sirro: Tumekatata Watuhumiwa 311 wa Dawa za Kulevya.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Simon Sirro akizungumza na wageni waliofika kwenye mkutano huo.

Mkutano maalum wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na viongozi wengine mbalimbali wa mkoa huo pamoja na waandishi wa habari, unafanyika Jana February 13,2017, kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere, Posta jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, Makonda alikabidhi majina 97  ya watuhumiwa wa madawa ya kulevya kwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Siang’a.

Akitoa ripoti ya oparesheni ya kwanza na pili ya kusaka watuhumiwa wa dawa za kulevya, Kamanda Sirro, amesema;

Taarifa ya operesheni tuliyoifanya wiki ya tatu iliyozinduliwa na Mkuu wa Mkoa Paul Makonda, lengo ni kuwakamata wote wanaojihusisha na biashara hii ya madawa ya kulevya. Mkuu wa mkoa aliunda kamati ya kufanya upelelezi.

Watuhumiwa waliokamatwa ni 311 na vielelezo. Kete 544 za heroin, Mirungi bunda 21.

Watuhumiwa 117 wamekutwa na vielelezo, 194 hawajakutwa na vielelezo.

“Watuhumiwa 77 walitakiwa kuja baada ya kutajwa na mkuu wa mkoa.

Hadi jana watuhumiwa 32 wameripoti na kuhojiwa, watuhumiwa 45 hawajaripoti na juhudi zinafanyika kuwapata.” Kamnada Sirro alisema.

Kamanda Sirro aliongeza kuwa, ambao hawajaripoti watasakwa popote walipo na kupelekwa mahakamani.

Watuhumiwa wengine upelelezi unaendelea. Pongezi za dhati kwa mkuu wa mkoa kwa ushiriki wake binafsi ya kuongoza mapambano haya. Ukishakuwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ni vizuri kwenda kwenye ground uone kazi zinazofanyika.

Wote waliotakiwa kufika kituo cha polisi na hawakufika, watatafutwa na watahojiwa, hilo halikwepeki.

“Kuna wengine wakubwa hawakuamini kama watalala mahabusu, ila walilala, tukikuhoji hatukuachii sababu utaharibu utaratibu.

“Hakuna mtu aliye juu ya sheria hata ukiwa na ukubwa kiasi gani. Nashukuru wengine wameanza kujisalimisha wenyewe.” Alimalizia Sirro.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad