UCHAGUZI ZANZIBAR :-Dk. Shein ashinda Kwa asilimia 91.4. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 21, 2016

UCHAGUZI ZANZIBAR :-Dk. Shein ashinda Kwa asilimia 91.4.

Mgombea wa urais kupitia chama cha CCM Visiwani Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein ameshinda kiti cha urais kwa jumla ya kura 299,982 awa na asilimia 91.4 ya kura zote halali 328,327 katika uchaguzi wa marudio uliofanyika jana,March 20,2016.

Matokeo hayo yametangazwa leo,March 21, 2016 na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha.

Uchaguzi huo wa marudio ulifanywa jana baada ya kufutwa Oktoba 25,2015 kutokana na kile kilichotangazwa na Jecha kuwa ni kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa taratibu za uchaguzi huo.
Uchaguzi huo ulisusiwa na vyama kumi kwa kile walichodai kuwa kufutwa kwa uchaguzi huo mwezi Oktoba ilikuwa ni batili.

Hata hivyo karatasi za kupigia kura zilikuwa na majina yote ya wagombea kama ilivyokuwa katika uchaguzi mkuu wa Oktoba,2015.

Jecha alifafanua kuwa hakuna hata mgombea mmoja aliyefuata utaratibu wa kujitoa kwa mujibu wa sheria na kanuni.
Matokeo yote kama yalivyotangazwa  yako  hapo  chini....

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad