MATOKEO / RATIBA VPL 2015/2016:-Yafahamu Marekebisho ya ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, March 24, 2016

MATOKEO / RATIBA VPL 2015/2016:-Yafahamu Marekebisho ya ratiba ya Ligi Kuu Tanzania Bara.

Marekebisho ya ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom ,VPL 2015/2016 yamezingatia mechi za viporo za timu za Azam FC na Yanga SC zinazoshiriki mashindano ya kimataifa (Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho).

Pia ushiriki wa Azam FC na Yanga SC katika mechi zijazo za mtoano (play offs) zinazokutanisha timu zitakazotolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika, na zile zilizosonga mbele kwenye Kombe la Shirikisho.

Iwapo Azam FC itasonga mbele itacheza mechi hizo za mtoano, wakati Yanga SC yenyewe itacheza tu mechi hizo za mtoano iwapo itatolewa katika raundi inayofuata ya Ligi ya Mabingwa. Hivi sasa Azam na Yanga zinashiriki hatua ya 16 bora ambayo itachezwa kati ya Aprili 8-10,2016 kwa mechi za nyumbani, na Aprili 19 na 20,2016 kwa mechi za ugenini.

Mechi za kwanza za raundi ya mtoano (play offs) zitachezwa kati ya Mei 6-8,2016 wakati za marudiano zitafanyika Mei 17-18,2016. Yanga SC ikiitoa Al Ahly maana yake haitacheza hatua ya mtoano (play offs), na badala yake itasubiri moja kwa moja hatua ya makundi ambayo mechi zake za kwanza zitafanyika kati ya Juni 17-19,2016.

Marekebisho mengine yanaweza kufanyika kwa kuzingatia matokeo ya scenario hizo hapo juu.

Wasalaam,

Boniface Wambura

Ofisa Mtendaji Mkuu

Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad