UCHUMI NA BIASHARA:-TCRA yavifunga vituo 21 vya habari Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, January 17, 2016

UCHUMI NA BIASHARA:-TCRA yavifunga vituo 21 vya habari Tanzania.

 Mamlaka ya mawasiliano nchini Tanzania, TCRA imevifungia vituo 21 vya Radio na 6 vya Television kwa muda wa miezi 3 kikiwemo kituo cha Star TV, Radio free Afrika, Kiss Fm na Uhuru FM.

Vituo hivyo vimefungiwa kutoa huduma kwa miezi mitatu kila moja baada ya kushindwa kulipa kodi.

Kulingana na mtandao wa jamii Forum,mnamo mwezi July 2015 Serikali ilitoa taarifa kwa umma na TCRA kwamba baadhi ya radio na Televisheni zipatazo 40 zinadaiwa ada na tozo mbalimbali.

 Aidha Serikali iliviagiza vituo hivyo kuhakikisha kuwa vimelipa ada kufikia tarehe 31 mwezi Disemba 2015.

Hatahivyo baadhi ya vituo hivyo vililipa kodi hiyo mwanzoni mwa mwezi huu na wengine wakishindwa kulipa.

Kwa mujibu wa sheria unaposhindwa kulipa kodi TCRA huchukulia kwamba haupo.

TCRA sasa inasema kuwa iwapo miezi mitatu ijayo itakamilika bila malipo hayo kufanywa basi italazimika kuchukua hatua zaidi kama vile kuwapokonya leseni wahusika.

Ni vituo 11pekee kati ya vituo vilivyokuwa vikidaiwa na mamlaka hiyo vilivyotiii agizo hilo na kulipa.

Baadhi ya vituo hivyo ambavyo havitakuwa hewani kufikia jumatatu,January 18, 2016 ni

1. Sibuka FM 

2. Breez FM 

3. Country FM 

4. Ebony FM 

5. Hot FM 

6. Impact FM 

7. Iringa Municipal TV 

8. Kiss FM 

9. Kitulo FM 

10. Kifimbo FM 

11. Mbeya City Municipal TV 

12. Radio 5 

13. Radio Free Afrika (RFA) 

14. Musa Television Network 

15. Pride FM radio 

16. Radio Huruma 

17. Radio Uhuru 

18. Star TV 

19. Rock FM Radio 

20. Standard FM radio 

21. Sumbawanga Municipal TV 

22. Tanga City TV 

23. Top Radio FM limited 

24. Ulanga FM

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630 .

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad