![]() |
Mwanajeshi
feki ( PICHANI) wa Jeshi la wananchi (JWTZ) amekamatwa November 02,2015, Mkoani Kigoma akiwa
amevaa sare za Jeshi hilo na
kuwatapeli fedha baadhi ya watu.
Akiongea na
waandishi wa habari ofisini kwake juu ya tukio hilo ,Kamanda wa Polisi wa Mkoa
wa Kigoma, Fednandi Mtui alisema kuwa mwanajeshi huyo feki alikamatwa eneo
la kazuramimba katika Wilaya ya uvinza.
Kamanda Mtui alisema
kuwa mwanajeshi huyo alitambulika kwa jina la James Charles miaka 27 mkazi wa
kijiji cha Nyamori, alikamatwa baada ya kuwepo kwa taarifa kutoka kwa raia wema
juu ya utapeli aliokuwa akiwafanyia na kuwekewa mtego na kukamatwa.
Kamanda
alisema kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kuhojiwa na kuulizwa alipozitoa sare hizo
alisema kuwa yeye ni dobi wa kufua nguo,hivyo huvaa sare hizo pale anapoletewa
na wateja kwa ajili ya kuzifua.
Amesema
mtuhumiwa huyo amekuwa akijifanya Ofisa wa JWTZ na Ofisa wa uhamiaji na
amekamatwa akiwa tayari amewatapeli wananchi shilingi Milioni Moja ambapo
alikuwa ameshachukua shilingi Laki moja kati ya hizo
Alisema
mtuhumiwa atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika,pia jeshi la polisi
limetoa wito kwa wananchi wote ambao wameshatapeliwa na mtuhumiwa huyo kutoa
taarifa katika kituo chochote cha polisi kilichopo jirani yao.
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo
na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia
tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Tuesday, November 03, 2015

SHERIA YETU:-Mwanajeshi feki akamatwa Mkoani Kigoma.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment