![]() |
Didier
Kavumbangu (kushoto) amefunga mabao mawili leo Azam FC ikishinda 5-0
Klabu ya Azam FC imerejea kileleni mwa Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara 2015/2016 baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Toto
Africans kwenye mchezo wake Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam
jioni ya leo November 01,2015.
Ushindi huo
unaifanya timu ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake
ifikishe (Azam FC) pointi 25 baada
ya kucheza mechi tisa, ikiwazidi kwa pointi mbili, mabingwa watetezi, Yanga SC
wenye pointi 23.
Shomary
Kapombe ndie aliefungua Mabao kwa kupachika Goli katika Dakika za 34 na 36 na
kisha Kipre Herman Tchetche kuipa Azam FC Bao la 3 kwenye Dakika ya 45.
Kipindi cha
Pili, Azam FC walifunga Bao la 4 baada ya Toto Africans kujifunga wenyewe na
Didier Kavumbangu kupiga Bao la 5.
MATOKEO
MECHI ZA LIGI KUU YA VODACOM TANZANIA BARA 2015/2016.
Leo; Novemba
01, 2015
Prisons 2 - 2
Ndanda FC
African
Sports 0 - 2 JKT Ruvu
Azam FC 5 - 0
Toto Africans
Jana; Oktoba
31, 2015
Simba SC 6 -1
Majimaji FC
Kagera Sugar
0 -2 Yanga SC
Mtibwa Sugar
4-1 Mwadui FC
Coastal
Union 1-1 Mbeya City
Kesho;
Novemba 02, 2015
Mgambo
Shooting Vs Stand United
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.
|
Sunday, November 01, 2015

Home
MICHEZO
LIGI KUU TANZANIA BARA 2015/2016:- Azam FC hao kileleni leo November 01,2015 wakimfunga Toto Africans 5 - 0.
LIGI KUU TANZANIA BARA 2015/2016:- Azam FC hao kileleni leo November 01,2015 wakimfunga Toto Africans 5 - 0.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment