KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2018:-Picha 12 za Taifa Stars walivyojiandaa kuikabili Algeria November 14 - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, November 05, 2015

KUFUZU KOMBE LA DUNIA 2018:-Picha 12 za Taifa Stars walivyojiandaa kuikabili Algeria November 14

Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars inayojiandaa kwa ajili ya mchezo wa kuwania kufuzu Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Algeria, imeendelea na mazoezi ya kujiweka sawa kuelekea mchezo huo utakaopigwa November 14 uwanja wa Taifa Dar Es Salaam na November 17 kurudiana Algeria.

 Kabla ya kucheza mchezo huo Taifa Stars itacheza mchezo mmoja wa kirafiki Jumapili ya November 8 dhidi ya timu ya chuo kikuu cha Pretoria  Tucks FC jijini Johannesuburg Afrika Kusini.
IMG_0029

IMG_0058
Kocha wa Taifa Stars Charles Mkwasa ameomba kucheza mchezo huo ili kupata nafasi ya kuangalia kikosi chake kabla ya mchezo na Algeria.

Taifa Stars wapo Johannesuburg Afrika Kusini kwa kambi ya siku 10 kabla ya kurejea Dar Es Salaam kucheza mechi dhidi ya Algeria, Stars inafanya mazoezi asubuhi na jioni kwa ajili ya kujiweka sawa na inatumia viwanja vya St. Peters College na kituo cha michezo cha Edenvale.

IMG_0043 (1)
IMG_0066
IMG_0039
IMG_0072
IMG_0086
IMG_0126
Kuhusu hali ya kambi, kocha mkuu wa Stars Charles Mkwasa amesema anashukru maendeleo ni mazuri vijana wake wote wapo katika hali nzuri hakuna majeruhi na wanaendelea na maaandalizi ya mchezo dhidi ya Algeria utakaopigwa Novemba 14 jijini Dar es salaam.

Wachezaji 26 waliopo kambini ni magolikipa Ally Mustafa, Aishi Manula na Said Mohamed, walinzi ni Shomari Kapombe, Juma Abdul, Ramadhan Kessy, Mohamed Hussein, Mwinyi Haji, Hassan Isihaka, Salim Mbonde, Kelvin Yondani na nahodha Nadir Haroub “Cannavaro”.
Wengine ni Himid Mao, Frank Domayo, Mudahir Yayha, Salum Abubakar, Said Ndemla, Jonas Mkude, Salum Telela, Farid Musa, Saimon Msuva, Malimi Busungu, Elias Maguri, John Bocco na Mrisho Ngasa.

Aidha wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea klabu ya TP Mazembe ya Congo DR, wanatarajiwa kuungana na kikosi cha Stars baada ya mchezo wao wa fainali Ligi ya Mabingwa Afrika Jumapili dhidi ya USM Alger.
IMG_0131
IMG_0124
IMG_0107
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad