![]() |
Taarifa hiyo
ilieleza kuwa viongozi hao wawili walikutana kwa takribani saa moja Ikulu,
kuzungumzia hali ya kisiasa Zanzibar kufuatia ombi la Maalim Seif kutaka
kukutana na kuzungumza na Rais Kikwete.
“Viongozi
hao wamekubaliana kuwa mashauriano yaendelee kufanyika baina ya pande zote
zinazohusika na hali ya kisiasa Zanzibar,” taarifa hiyo ilieleza kwa kifupi.
Zanzibar
inakabiliwa na mgogoro wa kisiasa, baada ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC)
kufuta matokeo ya Uchaguzi wa Rais na uwakilishi wa Zanzibar, kwa maelezo kuwa
ilibaini kuwapo kwa kasoro kadhaa kisiwani Pemba.
Uamuzi wa
kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika Oktoba 25, mwaka huu 2015 ulitangazwa
na Mwenyekiti wa ZEC, Jesha Salim Jecha, Oktoba 28, mwaka huu na kuibua
mgogoro.
Katika
tangazo la kufuta matokeo hayo, Jecha alisema uchaguzi huo utarudiwa, lakini
Maalim Seif, viongozi na wafuasi wa CUF wanapinga kurudiwa kwa uchaguzi huo na
kusisitiza kwamba Maalim Seif anapaswa kuapishwa.
Waangalizi
wa kimataifa na wa ndani pia walieleza kushangazwa kwao na hatua ya Jecha
kufuta matokeo hayo wakati hawakushuhudia kasoro zozote wakati wa upigaji kura
kisiwani Pemba hadi baada ya kutoa taarifa yao ya kwanza.
Mataifa
kadhaa ya nje yakiwamo Uingereza, Ireland na Marekani pia yalieleza kushangazwa
na uamuzi wa wao na kushauri ZEC iendelee na mchakato wa kutangaza matokeo.
Hata hivyo,
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetoa taarifa za kukubaliana na uamuzi wa Zec wa
kufuta matokeo na kutaka uitishwe uchaguzi mpya.
Kabla Maalim
Seif, ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar hajakutana na Rais Kikwete jana, alilalamika
kwamba alikuwa akiwapigia simu pamoja na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed
Shein, bila kuzipokea kwa lengo la kutaka kutafuta suluhisho la mgogoro huo.
Wadau kadhaa
wameshaingilia kati kusaka suluhu kwa kukutana na pande zinazohusika. Miongoni
mwao mi Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, viongozi wa dini na
viongozi wastaafu.
Source:-Nipashe.
Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER , INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp .
|
Thursday, November 05, 2015

HALI YA SIASA ZANZIBAR:- Rais Kikwete ateta na Maalim Shariff Seif Hamad.
Tags
# SIASA
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
SIASA
Labels:
SIASA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment