Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania bara -NEC, Jaji Mstaafu Damian Lubuva
amemkabidhi cheti cha ushindi wa kiti cha URAIS, Dk John Pombe Magufuli na
mgombea mwenza wake, Bi.
Samia Suluhu katika
Ukumbi wa Diamond Jubilee
asubuhi ya leo hii October
30,2015.
Katika tukio
hilo, Wagombea urais wa Chadema Edward Lowassa na Hashim Rungwe wa
Chauma wamesusia sherehe hizi za
kukabidhiwa cheti cha ushindi Dk John Magufuli wa CCM.
Mwenyekiti
wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania Jaji Mstaafu Damian Lubuva alisema kuwa
Magufuli, alijipatia kura 8,882,935 ikiwa ni aslimia 58.46.
Mpinzani
wake wa karibu Edward Lowassa wa chama cha Chadema alijipatia kura 6,072,848
ikiwa ni asilimia 39.97 ya kura zote halali.
Baada ya
kutangazwa kwa ushindi wake, wafuasi wake walisherehekea katika miji mbalimbali
nchini humo.
|
No comments:
Post a Comment