LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA 2015/2016:- Azam FC haoo waishusha Yanga SC kwa ushindi wa 4-2 leo October 29,2015. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, October 29, 2015

LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA 2015/2016:- Azam FC haoo waishusha Yanga SC kwa ushindi wa 4-2 leo October 29,2015.




Didier Kavumbangu (kushoto) akishangilia na Farid Mussa baada ya kufunga bao la kwanza leo October 29,2015.



Klabu ya Azam FC imefanikiwa kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2015/2016 baada ya kuifunga JKT Ruvu mabao 4-2 jioni ya leo October 2015,kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
Ushindi huo unaifanya timu hiyo ya Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na familia yake kufikisha pointi 22 baada ya kucheza mechi nane, ikiwazidi pointi mbili mabingwa watetezi, Yanga SC ambao jana October 28,2015,walilazimishwa sare ya 2-2 na Mwadui mjini Shinyanga.

Kwa ushindi wa leo, sifa zimuendee mshambuliaji Mrundi, Didier Kavumbangu ambaye amefunga bao moja na kuseti mengine mawili, moja la John Bocco na lingine la Kipre Tchetche. 


Didier Kavumbangu akipiga shuti kufunga bao la pili pembeni ya beki wa JKT Ruvu, Michael Aidan
MATOKEO YA LIGI KUU YA VODACOM TZ BARA
Oktoba 29, 2015.

Prisons  1-0 African Sports

JKT Ruvu  2-4 Azam FC

Oktoba 28, 2015.

Toto African 1-0 Mgambo Shooting

Mwadui FC 2-2 Yanga SC

Mtibwa Sugar 1-0 Kagera Sugar

Mbeya City 1-1 Majimaji FC

Ndanda FC 0-0 Stand United

Simba Sc  1-0 Coastal Union

Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.






No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad