AJALI / PICHA:-Tazama Jinsi Treni ya Abiria ikiacha Njia Mjini Shinyang’a huku abiria zaidi ya 150 wakikumbwa na Taharuki. - Mwana Wa Makonda
cV7ufzj

Muhtasari

X-BET

MAIN-

Post Top Ad

cV7ufzj

Thursday, September 10, 2015

demo-image

AJALI / PICHA:-Tazama Jinsi Treni ya Abiria ikiacha Njia Mjini Shinyang’a huku abiria zaidi ya 150 wakikumbwa na Taharuki.

.com/simgad/
A
Hapa ni katika eneo la Station mjini Shinyanga treni ya abiria ikiwa imeacha njia( haionekani vizuri hapo chini) na kusababisha abiria 159 wanaosafiri na treni hiyo kutoka Tabora kwenda jijini Mwanza kunusurika kufa na kukwama kwa saa kadhaa....Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog –Shinyanga.

B
Tukio hilo limetokea leo September 10,2015,asubuhi baada ya kichwa cha treni hiyo kutoka kwenye njia ya reli na mabehewa ya treni kuanza kukanyaga mataluma na kusababisha adha kwa abiria hao.

Mkuu wa kituo cha reli (Station Master) Shinyanga,Bw. Baruani Issa amesema katika treni hiyo kulikuwa na abiria 159 na kwamba ajali hiyo imetokea kutokana na miundo mbinu ya reli kuwa chakavu.

Station Master huyo amesema utaratibu uliofanywa na Shirika hilo ni kufanya utaratibu wa kuwarudishia nauli abiria hao ili wapande mabasi na kuendelea na safari zao ili kupunguza usumbufu wakati utaratibu wa matengenezo unafanyika ili treni iendelee na safari zake kama kawaida.

Wakizungumza na Waandishi wa Habari,Baadhi ya  abiria waliokuwa wanasafiri na treni hiyo mbali na kumshukuru mwenyezi mungu kwa kuwanusuru na ajali hiyo wameiomba serikali kuboresha miundo mbinu ya reli kwani asilimia kubwa ya Watanzania wanategemea usafiri huo wenye gharama nafuu.
C
Treni ikiwa imesimama.....Papo kwa Papo >>>> Pata Picha, Habari za  Siasa, Kijamii, Biashara, Muziki na Michezo na Nyingine kwa kujiunga  na mimi hapa…..FACEBOOK , TWITTER INSTAGRAM , Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Contact Form

Name

Email *

Message *