OCTOBER 02,2014:-Na Historia ya Maisha ya Msani Diamond Platnumz. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, October 04, 2014

OCTOBER 02,2014:-Na Historia ya Maisha ya Msani Diamond Platnumz.

Ukitaka kujua kuwa ku-shine hapa Bongo ni juhudi zako tu mwenyewe za kupiga kazi usiku na mchana bila kulala na mwisho wa siku kufikia malengo yako basi mfano wa kuigwa ni huyu Birthday boy Diamond Platnumz.

Diamond alizaliwa tarehe 02, October mwaka 1989 katika Hospitali ya Amana Dar es salaam   mnamo wa saa kumi na moja na kupewa jina la  Nasibu Abdul Juma .
Akiwa na umri mdogo wazazi wake walitengana na baba yake kumuacha bila msaada wowote  na ikabidi wahamie Tandale Magharibi kwa bibi  yake mzaa mama, na hapo ndipo yakawa makazi yao.

Historia yake ni ya kusikitisha kama alivyoelezea kwenye wimbo wa binadamu wabaya.

Mnamo mwaka 1995  alianza kupata elimu ya Nursery katika shule ya Chakula Bora iliyopo  Tandale Uzuri hadi alipomaliza na kujiunga na Elimu ya Msingi yaani  (Primary School) mwaka 1996 katika shule ya msingi Tandale magharibi  iliyopo jijin Dar-es-salaam.

Ilipofika mwaka 2000 akiwa darasa la tano  diamond alionekana kuanza kupenda sana muziki, hivyo alianza kucopy  baadhi ya na kukrem nyimbo za wasanii waliokuwa wakihit ndani na nje ya  nchi kwa kipindi hicho na kuwa anaimba katika sehem tofautitofauti.

Karibu kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana /Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad