CHUKUA TAHADHARI:- Kisa hofu ya kuibiwa….Jenereta lawaua Baba,Mama na Watoto wote. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, October 05, 2014

CHUKUA TAHADHARI:- Kisa hofu ya kuibiwa….Jenereta lawaua Baba,Mama na Watoto wote.

Miili ya watoto watatu wa familia hiyo.

 Mume, Mke na Watoto wao watatu wamefariki dunia baada ya kupumua hewa iliyojaa gesi ya “carbon monoxide” iliyokuwa ikitolewa na generator waliloliwasha ndani ya nyumba yao .

Katika tukio hilo la kusikitisha,limetokea Lagos, Nchini Nigeria ambapo miili ya wahanga wote watano iligunduliwa na majirani zao. 

Majirani wameripoti kuwa baba wa familia hiyo alinunua generator siku mbili kabla ya kukutwa na umauti, na kuliweka chumbani kwake akihofia kuwa litaibwa akiliweka nje.
Siku iliyofuatia, majirani waligundua kuwa wanafamilia hao wote walikuwa kimya, na ndani ya nyumba yao siku nzima, hivyo mmoja wao akaamua kuangalia kujua kinachoendelea. 

Jirani huyo aliona miili ya marehemu na kuwataarifu wenzake. Walipoingia ndani ya nyumba, walistushwa na janga walilokutana nalo.
Mwili wa mama, na wa mmoja wa watoto unaonekana kwa mbali nyuma yake.

Aidha  moshi unaotolewa na Jenereta, mfano kama  mkaa, magari, pikipiki, na mashine nyingi, kuna gesi ya “carbon monoxide (CO)” ambayo, ni sumu inayokusababisha mwili wa Binadamu kama ikivutwa kuchoka, kupoteza fahamu, na hatimaye kufariki taratibu bila onyo, maumivu, wala kujijua. 

Utadhani unapata usingizi na kujilaza, kumbe ndio mauti yanakukuta. Uthithubutu kupika kwa kutumia mkaa ndani ya nyumba bila kufungua madirisha, au kuwasha jenereta ndani ya nyumba, au kuwasha gari katika “garage” wakati madilisha na milango imefungwa; maana hiyo ni sawa na kucheza na kifo. 

Gesi ya Carbon Monoxide ni tofauti na Carbon Dioxide (CO2) inayopumuliwa na wanyama, ambayo si sumu na inatumiwa na mimea katika photosynthesis.
Karibu kwenye familia ya Makonda Blog na uzipokee Picha/Habari zote kwa kutumiwa Mchana /Usiku baada tu ya kujiunga kwa kubonyeza hapa mtu wangu >>>BONYEZA HAPA.>>>Pia tutumie tukio la Picha kwa WhatsApp +255789925630.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad