Historia fupi ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Dr. William Mgimwa aliyefariki dunia nchini Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, January 01, 2014

Historia fupi ya Waziri wa Fedha wa Tanzania, Dr. William Mgimwa aliyefariki dunia nchini Afrika Kusini alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

 Kuzaliwa:-Januari 20, 1950 Kalenga mkoani Iringa…Elimu:
1966 - 1967 Shule ya Msingi Tosa
1961 -1965 Shule ya Msingi Wasa
1970-1971 Seminari ya Mafinga
1968 - 1969 Tosamaganga Sekondari
1975 - 1984 Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) - Postgraduate in Finance
1989 - 1991 IDM Mzumbe (MBA - Finance)


Waziri wa Fedha William Mgimwa ,
enzi za uhai wake.

Waziri wa Fedha, ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kalenga, Iringa, William Mgimwa amefariki dunia leo(Januari 01,2014) akiwa hospitali ya Mediclinic Kloff, Afrika Kusini alipokuwa akitibiwa!

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue, ambaye amesema Mgimwa amefariki majira ya saa 5:20 saa za Afrika Kusini ambapo ni sawa na saa 6:20 kwa majira ya Tanzania.

Marehemu Mgimwa alizaliwa Januari 20, 1950 na amefariki akiwa na umri wa miaka 63.

Alipata Stashahada ya Juu (Advanced Diploma) na Stashahada ya Uzamili (Postgraduate Diploma) katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es Salaam.

Alisoma Shahada ya Uzamili katika Usimamizi wa Fedha (MBA) katika Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad