Tazama muonekani wa Banda linaloendelea kujengwa katika eneo la makazi ya Hayati Mzee Nelson Mandera kwa ajili ya maandalizi ya shughuli za maziko wiki hii. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 09, 2013

Tazama muonekani wa Banda linaloendelea kujengwa katika eneo la makazi ya Hayati Mzee Nelson Mandera kwa ajili ya maandalizi ya shughuli za maziko wiki hii.

Hili ni Banda linaloendelea kujengwa katika eneo la makazi ya Hayati Mzee Nelson Mandera kwa ajili ya maandalizi ya shughuli za maziko yanayotarajia kufanyika mwishoni mwa wiki hii(Desemba 15,2013), ....ambapo zaidi ya viongozi 70 wa mataifa makubwa, kutoka pande zote za dunia wanatarajia kuhudhuria maziko hayo.

Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini ameaga dunia(Desemba 05,2013) . Mandela ameaga akiwa na umri wa miaka 95 na yeye ndiye aliongoza Afrika Kusini kutoka mikononi mwa watawala wa enzi ya ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini baada ya kufungwa jela kwa miaka 27
Mandela alikua anpokea matibabu ya homa ya mapafu nyumbani kwake baada ya kulazwa hospitalini kwa miezi mitatu.


Mnamo mwaka 2005, Mandela alitangaza kwa taifa kua mwanawe wa kume alifariki kutokana na ugonjwa wa Ukimwi.Katika taarifa yake kwa watu wa Afrika Kusini, Rais wa taifa hilo, Jacob Zuma , alisema kuwa Mandela amewaaga lakini yuko mahali salama.

Rais Zuma amesema kuwa taifa limepoteza mtu waliyemjua kama mtoto wa taifa hilo.

Mandela aliwahi kushinda tuzo ya amani ya Nobel, na kutambulika kama rais aliyeheshimika sana hasa kwa kupatanisha watu wa Afrika Kusini baada ya kuondoka gerezani.

Hakuonekana sana hadharani tangi alipostaafu mwaka 2004.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad