Taswira ya Ajali ya Basi la HOOD iliyoua mtu mmoja na Kujeruhi 27 mkoani Morogoro Jana. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, December 20, 2013

Taswira ya Ajali ya Basi la HOOD iliyoua mtu mmoja na Kujeruhi 27 mkoani Morogoro Jana.


Wananchi wakilishuhudia Basi la kampuni ya Hood Limited aina ya Scania lenye namba za usajili T 159 AXM baada ya kupinduka kwenye kona kali iliyopo eneo la Melela, Mlandizi wilayani Mvomero, Morogoro jana (Desemba 19,2013) lililokuwa likitoka jijini Mbeya kueleka Arusha limepinduka majira ya saa nane mchana na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi 27.



Gari hilo baada ya kupinduka.…



Baadhi ya abiria waliokuwa wanasafiri katika basi hilo.



Baadhi ya abiria wakitoa mizigo yao katika basi hilo.



Basi hilo likitolewa eneo la ajali.


Baadhi ya wananchi wakipanda basi lingine la Hood kuendelea na safari kama kawaida.


...Baada ya kutolewa.


Eneo la Melela Mlandizi ilipotokea ajali hiyo.


Basi la kampuni ya Hood Limited aina ya Scania lenye namba za usajili T 159 AXM lililokuwa likitoka jijini Mbeya kueleka Arusha limepinduka kwenye kona kali iliyopo eneo la Melela, Mlandizi wilayani Mvomero, Morogoro jana (Desemba 19,2013) majira ya saa nane mchana na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi 27.

Majeruhi kadhaa katika ajali hiyo wamekimbizwa katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu.

Mashuhuda wa ajali hiyo walidai kwamba chanzo chake ni dereva wa lori aliyejaribu kulipita gari lingine kwenye kona hiyo.

"Mimi nilikuwa natoka Mbeya naenda Moshi kwa ajli ya sikukuu ya Krismas, dereva wetu amefanya kazi kubwa sana ya kuokoa maisha yetu.

"Tulipofika hapa kwenye kona, dereva wetu baada ya kuona lori limejaa upande wetu akaamua kukwepa kugongana nalo uso kwa uso na kuingia huku lilipo. Binafsi nampa pongezi nyingi dereva wa hili basi letu" alisema Bi. Ruth Mwambogoso abiria katika basi hilo

(PICHA NA DUSTAN SHEKIDELE / GPL, MORORGORO)

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad