Hongera Padre Lazaro Paul Kadende kwa kutimiza Miaka 50 ya kumtumikia Mungu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, December 19, 2013

Hongera Padre Lazaro Paul Kadende kwa kutimiza Miaka 50 ya kumtumikia Mungu.

Waumini wa kanisa katoliki Jimbo la Rulenge Ngara mkoani Kagera Jana(Desemba 18,2013) waliungana na Padre Lazaro Kadende wa Jimbo hilo kuadhimisha miaka 50 ya upadre katika sherehe iliyofanyika katika Parokia ya Buhororo wilayani Ngara mkoani Kagera.

(Kutoka kulia)Ni Baba askofu wa Jimbo la Rulenge Ngara Mhashamu Severini Niwemugizi pamoja na mambo mengine ametoa wito kwa wazazi na walezi Jimboni humo kuwapa moyo watoto wao kuwa na miito ya utume kwa kuwapatia mafunzo ya imani kupitia kwa walimu wa kiroho.
Padre Sumbuso amesema kuwa waumini wanaunga na kiongozi wao kuadhimidha miaka 50 ya upadre ili kutafakari ufanisi wake katika Nyanja za elimu ,Uongozi na matumizi bora ya madaraka katika kutetea na kulinda haki za binadamu.


Padre Lazaro Kadende alizaliwa katika kijiji cha Nakatunga wilayani Ngara mwaka 1934 na kujiunga na elimu ya msingi mwaka 1944 ambapo mwaka 1945 alibatizwa kisha kujiunga na seminari mwaka 1947 huko Rubya wilayani Muleba na kuendelea 1957 huko Katigondo ya Bukoba.

Mnamo Januari 1963 alipewa daraja la ushemasi na na mhashamu askofu Joseph Kiwanuka na tarehe 18 Desemba 1963 alipata daraja la Upadre na kuanza harakati za kumtumikia Mungu na kuchunga kondoo wake kwa njia za kiroho.

Aidha  Padre Lazao Kadende katika utumishi wa daraja la upadre ametumikia parokia mbalimbali za jimbo la Rulenge Ngara na kuwa mkurugenzi wa elimu jimboni ,mkurugenzi wa vipindi vya radio na makamu wa baba Askofu

Nae Baba askofu wa jimbo la Rulenge Ngara ,Mhashamu Severini Niwemugizi ametoa wito  kwa wazazi na walezi kuwapa moyo watoto wao kuwa na miito ya utume kwa kuwapatia mafunzo ya imani kupitia kwa walimu wa kiroho.

Amesema kuwa vijana pia watumie elimu na vipaji waliojaliwa na mungu bila kulazimishwa walitumikie kanisa kwani kazi ya kulitangaza neon la Mungu ni kama kazi nyingine na mafanikio yake yanajengwa na upendo kuhubiri amani na subira.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad