PICHA:- Majambazi watatu waliouwawa na Polisi waliokuwa wakipanga kuvamia mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu uliopo wilayani Kahama. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, December 20, 2013

PICHA:- Majambazi watatu waliouwawa na Polisi waliokuwa wakipanga kuvamia mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu uliopo wilayani Kahama.

Kamanda Mangala amesema miili ya Majambazi hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya ya Kahama…na kwamba mbali na kukutwa na mabomu hayo ya kivita pia wamekutwa na bunduki mbili za kivita aina ya SMG zenye namba za usajili 1972PX7482 na UC-17751998 pamoja na risasi 94 ndani ya magazine nne.


Majambazi ambao majina yao hayajafahamika waliokuwa wakipanga kuvamia mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu uliopo wilayani Kahama usiku wa kuamkia leo(Desemba 20,2013).

Wakiwa mochwari hospitali ya wilaya ya kahama


Watu watatu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi, wameuawa kwa kupigwa risasi na polisi katika kijiji cha Namba Tisa kata ya Bulyanhulu Tarafa ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga wakati wakiwa katika harakati za kufanya uhalifu kwenye mgodi wa dhahabu wa  Bulyanhulu.

Watu hao ambao hawajafahamika majina yao, wana umri wa kati ya miaka 25 na 30.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, Evarist Mangala (pichani), alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia jana wakati watuhumiwa hao wakiwa katika harakati za kuvamia mgodi wa dhahabu Bulyanhulu.

Kamanda Mangala alisema wakati watu hao wakiwa katika harakati za kufanya uhalifu huo, walianza kurushiana risasi na polisi.

Hata hivyo, alisema watu hao walizidiwa nguvu na polisi na kusababisha vifo vyao.

Kamanda Mangala alifafanua kuwa baada ya kuwaua watuhumiwa hao, polisi walikamata silaha za kivita yakiwamo mabomu matatu ya kurushwa kwa mkono na bunduki mbili aina ya Sub Machine Gun (SMG) zenye namba 1972px7482 na ya pili yenye namba UC-17751998 pamoja na risasi 94 zikiwa kwenye magazine nne.

Alisema watu hao wanadaiwa walipanga kupora mali katika mgodi huo lakini walikwama baada ya polisi kupewa taarifa kutoka kwa wanakijiji na kufika eneo hilo.

Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga,
Evarist Mangala
Kamanda Mangala aliongeza kuwa baada ya kufika eneo la tukio, watuhumiwa hao walianza kurushiana risasi na polisi lakini walizidiwa nguvu na kuuawa wote.

Aidha, alisema miili ya majambazi hao imehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kahama ikisubiri kutambuliwa na ndugu zao.

Alitoa wito kwa wananchi mkoani humu kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa pale wanapohisi kutokea uhalifu ili kudhibiti matukio hayo mapema.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad