Manchester United yapigwa kipigo mfululizo huku Stoke City nayo ikimshitua Chelsea kwa bao 3-2. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, December 07, 2013

Manchester United yapigwa kipigo mfululizo huku Stoke City nayo ikimshitua Chelsea kwa bao 3-2.

Wadadisi wa Soka wanasema ikiwa Manchester United itaendelea kushindwa michezo yake ya Ligi kuu Uingereza (EPL)huenda isiwe katika nafasi za kwanza hadi nne katika Msimamo wa Ligi.

Haiwezekani: David Moyes  kocha wa Manchester United akiukwepesha mpira ili Hatem Ben Arfa asiuchukue,Unaweza sema  kuwa na msimu mbaya baada ya kupigwa bao 1-0 katika mechi iliyomalizika muda mfupi uliopita kwenye Uwanja wa Old Trafford wakati ilipokuwa ikipambana na Newcastle United katika mchezo wa Premier.
Kipingo hicho ambacho ni cha tano kimeifanya Man United iwe na msimu mbaya kuliko yote ndani ya kipindi cha miaka 20 iliyopita, ambapo Jumatano iliyopita, United ilifungwa bao 1-0 na Everton katika ligi hiyo.


Manchester United Jumamosi (Desemba 07,2013) lipata kipigo chake cha pili nyumbani katika muda wa siku nne baada ya kulazwa bao moja bila na New Castle.

Mchezaji wa New Castle Yohan Cabaye ndiye aliipatia kilio Manchester United huku kwao ikiwa kicheko baada ya kushinda Manchester United kwa mara ya kwanza nyumbani Old Trafford tangu mwaka 1972.

Man United  walikuwa na wakati mgumu kuvunja ari ya Magpies na kukosa nafasi kadhaa za mabao mfano Patrice Evra alipogonga lango huku mpira ukirudi na kumgonga mkono Vurnon Anita.

Mpira wa kichwa wa Robin van Persie haukuzaa matunda kwa Manchester United,lakini Newcastle waliishia na kicheko baada ya kupata ushindi wao wa kihistoria dhidi ya Man United.

Bila shaka hii inazua wasiwasi mkubwa kwa David Moyes kwani Man U wanaendelea tu kudidimia kwa mabao.

Man United  wameshuka ngazi hasa baada ya kupata kipigo mara mbili mfululizo tena nyumbani Old Trafford ikiwa ni mara ya kwanza kwa hali hii kushuhUdiwa kwa United.

Mnamo Jumatano walilazwa na Everton huku wakiwa nyuma ya Arsenal kwa pointi 12 wakikabiliwa na tisho la kutokuwa katika msitari wa mbele kuwania kombe la ligi ya Premier.

Ikiwa wataendelea kushindwa hivi Man U hata huenda wasiwe katika nafasi za kwanza hadi nne katika msimamo wa Ligi.


Oussama Assaidi scored a superb late winner as Stoke City came from behind to stun Chelsea and earn just their fourth Premier League win this season.
Manchester United 0-1 Newcastle
 
Southampton 1 – 1 Manchester City,

Liverpool 4 – 1 West Ham United, 

Stoke City 3 – 2 Chelsea

West Brom 0 - 2 Norwich 

Palace 2 – 0 Cardiff

1 Arsenal 14 19 34
2 Liverpool 15 16 30
3 Chelsea 15 13 30
4 Man City 15 26 29
5 Everton 14 9 27
6 Newcastle 15 -1 26
7 Tottenham 15 -2 25
8 Southampton 15 5 23
9 Man Utd 15 3 22
10 Aston Villa 14 0 19
11 Swansea 14 1 18
12 Stoke 15 -5 17
13 Hull 14 -6 17
14 Norwich 15 -14 17
15 West Brom 15 -4 15
16 Cardiff 15 -11 14
17 West Ham 15 -6 13
18 Crystal Palace 15 -12 13
19 Fulham 14 -14 10
20 Sunderland 15 -17 9

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad