![]() |
Wachezaji wa
Stars wakimbeba Kipa wa Kilimanjaro Stars, Ivo Mapunda baada ya kuokoa penaltri
ya Dani Sserunkuma wa Uganda.
|
Mbali na
kuokoa penalti hizo mbili, Uganda walipoteza penalti nyingine moja baada ya
Godfrey Walusimbi kupiga, wakati Hamisi Kiiza Emannuel Okwi ndiyo pekee
walioifungia Cranes penalti.
Penati za
Kili Stars zilifungwa na Kevin Yondan, Athumani ‘Chuji’na Erasto Nyoni huku
Samatta na Kiemba wakipoteza Penati zao.
JE WAJUA?
- Uganda wametwaa Chalenji Cup mara 13 na Tanzania
Bara mara 3.
- Uganda waliitoa Kilimanjaro Stars 3-0 kwenye Nusu
Fainali Mwaka Jana.
- Mara zote 3 Tanzania Bara ilipotwaa Chalenji Cup
imekuwa ikiifunga Uganda.
Mwaka
1974 waliitoa kwa Penati 5-3 baada Sare ya 1-1,
1994 waliifunga 4-3 kwa Penati baada Sare ya 2-2 na Mwaka 2010 kwa Penati 3-2
baada Sare ya 0-0.
Katika Mechi
hiyo, Uganda walitangulia kufunga katika Dakika ya kwa Bao la Sserunkuma lakini
Mrisho Ngassa, akipokea pande toka Mbwana Samatta, alisawazisha katika Dakika
ya 21 na Ngassa tena kupiga Bao la Pili katika Dakika ya 38 kwa frikiki baada
Samatta kuchezewa Rafu.
Refa Wish
Yabarow wa Somalia aliipa pigo Kilimanjaro Stars katika Dakika ya 53 kwa kumtoa
kwa Kadi Nyekundu Kiungo Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Katika
Dakika ya 73, Uganda walisawazisha baada ya Kona iliyomkuta Martin Mpuga na
kufunga.
![]() |
Mshambuliaji wa Kenya, Haambee Stars, Jacob Keli akiwatoka mabeki wa Rwanda, AmavubiBayisenge Emery kulia na Tubane James kushoto Uwanja wa Manispaa, Mombasa leo(Desemba 07,2013). |
Sasa Tanzania
Bara, Kilimanjaro Stars itamenyana na wenyeji, Kenya, Harambee Stars katika
Nusu Fainali ya Kwanza ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA
Challenge Desemba 10, mwaka huu Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.
Hiyo
inafuatia Kenya kuifunga Rwanda 1-0 katika Robo Fainali ya pili CECAFA
Challenge jioni hii Uwanja wa Manispaa, Mombasa Kenya, bao pekee la beki wa
Azam FC ya Dar es Salaam, Joackins Atudo kwa penalti dakika ya 56.
Mapema katika Robo Fainali ya kwanza, Stars iliwatoa mabingwa watetezi, Uganda kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 2-2 ndani ya dakika 90.
Robo Fainali nyingine zitachezwa kesho(Desemba 08,2013), Ethiopia na Sudan na Zambia na Burundi, Uwanja wa Manispaa pia.
RATIBA/MATOKEO 2013/2014.
SIKU |
NA |
ROBO FAINALI |
MJI |
SAA |
Jumamosi Desemba 7 |
19 |
Uganda 2 Kili Stars 2 -Stars wasonga Penati 3-2 |
Mombasa |
1400 |
20 |
Kenya v Rwanda |
Mombasa |
1600 |
|
Jumapili Desemba 8 |
21 |
Zambia v Burundi |
Mombasa |
1400 |
22 |
Ethiopia v Sudan |
Mombasa |
1600 |
No comments:
Post a Comment