Manchester City kwa FC Barcelona, Arsenal kwa Bayern hapatoshi Ulaya 2013/2014:- hatua ya 16 bora. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, December 17, 2013

Manchester City kwa FC Barcelona, Arsenal kwa Bayern hapatoshi Ulaya 2013/2014:- hatua ya 16 bora.



Arsenal iliifunga Bayern Munich 2-0 mwezi Machi, lakini waliondolewa kwa sheria ya bao la ugenini msimu uliopita katika robo fainali baada ya kunyukwa 3-1 kwenye mchezo wa kwanza na Bayern pia imeiondoa Gunners kwenye mashindano hayo mara mbili kila walipokutana kwenye hatua ya mtoano.

Manchester City watakuwa na kibarua kizito mbele ya Barcelona katika  mechi za mtoano hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Arsenal wenyewe watakuwa na kazi nzito mbele ya bingwa mtetezi Bayern Munich ikiwa ni marudiano ya hatua hiyo ya msimu uliopita.

Kocha Arsene Wenger alisema “Katika miaka minne au mitano iliyopita tumekuwa na wakati mgumu kila tunapoingia kwenye hatua hii, labda wakati huu tutakuwa na bahati.”

Chelsea mabingwa wa 2012 wenyewe wametupwa kwa Galatasaray wakati mabingwa wa England,  Manchester United watajiuliza upya mbele ya Olympiakos ya Ugiriki.

Michezo mingine ya hatua hiyo itawakutanisha mabingwa mara saba AC Milan dhidi ya Atletico Madrid, Bayer Leverkusen dhidi ya Paris St-Germain, Schalke wametupwa kwa Real Madrid na Zenit St Petersburg wataonyeshana kazi na Borussia Dortmund.

City iliichapa Bayern Munich 3-2 katika mchezo wa mwisho wa Kundi D wangeweza kumaliza vinara wa kundi hilo kama wangeshinda 4-2.

Kocha wa Manuel Pellegrini hana wasiwasi sana na Barcelona ya sasa, lakini anajua kwamba anakazi kubwa ya kufanya kuhakikisha Manchester City wanarudia katika upangwaji wa ratiba nyingine hapo Machi jijini Nyon.

Mkurugenzi wa City, Ferran Soriano na mkurugenzi wa ufundi, Txiki Begiristain wote wamefanya kazi Barcelona na ndio waliomuuza Yaya Toure kwa City 2010.

Arsenal iliifunga Bayern Munich 2-0 mwezi Machi, lakini waliondolewa kwa sheria ya bao la ugenini msimu uliopita katika robo fainali baada ya kunyukwa 3-1 kwenye mchezo wa kwanza.

Bayern pia imeiondoa Gunners kwenye mashindano hayo mara mbili kila walipokutana kwenye hatua ya mtoano.

Mechi ya kwanza ya 16 bora zitachezwa kati ya Februari 18 na 19 kwa vinara wa makundi yote kuwa nyumbani wakati mechi za marudiano zitafanyika Februari 25 na 26.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad