Uzinduzi huo unafanyika siku moja baada ya mwili wa Nelson Mandela
kuzikwa katika kijiji cha Qunu, imezinduliwa kumbukumbu nyingine ambayo ni
sanamu kubwa yenye futi 30 iliyopewa jina la Nelson Mandela Unity Statue.
Rais wa Afrika ya kusini, Bw.Jacob Zuma, amewaongoza viongozi mbali mbali wa serikalini na familia ya Nelson Mandela kuzindua rasmi sanamu hiyo mpya ya Mandela ambayo inatajwa kuwa kubwa zaidi duniani, na itakua na urefu wa zaidi ya mita 9.
Uzinduzi wa sanamu hiyo umeenda sambamba na siku maalumu ya upatanishi, kukumbuka tukio la mwaka 1838
ambapo jeshi la Voortrekkers lilipigana na kulishinda jeshi la jamii ya Wazulu.
Katika vita hivyo, watu zaidi ya 100 walipoteza maisha, na baadae jeshi
hilo liliondoka kwenye ardhi ya watu kutoka jamii ya Wazulu.
Tukio la pili kwa tarehe hii ya leo ni lile la mwaka 1961, wakati chama
cha ANC kiliunda jeshi lake ambalo lilijulikana kwa jina la Umkhonto we Sizwe
dhidi ya utawala wa Frederik de Klerk kwa kukabiiana na ubaguzi wa rangi.
Siku hii ya mapumziko nchni Afrika ya kusini ilitangazwa rasmi na Nelson
Madiba Mandela, baada ya kutangazwa kua rais wa Afrika ya kusini tarehe 10 may
1994.
No comments:
Post a Comment