Luis Suarez na mabao 16 katika EPL msimu huu hadi kufukuzwa kazi Meneja Andre Villas-Boas. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, December 17, 2013

Luis Suarez na mabao 16 katika EPL msimu huu hadi kufukuzwa kazi Meneja Andre Villas-Boas.

Luis Suarez, Jana (Desemba 15,2013) akivaa utepe wa Nahodha, aliifungia Liverpool Bao 2 na kufikisha mabao 16 katika EPL msimu huu, walipoibonda Tottenham waliokuwa kwao White Hart Lane Bao 5-0 na kuikamata Nafasi ya Pili ya Ligi Kuu England wakiwa Pointi 2 tu nyuma ya Vinara Arsenal.



'I am not a quitter' - Villas-Boas.
Klabu ya Tottenham Jana(Desemba 16,2013)  imemfukuza kazi Meneja wao Andre Villas-Boas mara baada ya Jana kunyukwa Bao 5-0 na Liverpool.

Kipigo hicho cha ndio kimekuwa kisago kikubwa kwa Timu hiyo kwa Miaka 16 Uwanjani kwao White Hart Lane na kimewaacha wakiwa Nafasi ya 7 kwenye Ligi Kuu England wakiwa Pointi 8 nyuma ya Vinara Arsenal.

Villas-Boas, Miaka 36, aliteuliwa Meneja Tottenham Julai 2012.

Mwezi Machi 2012, Villas-Boas alifukuzwa kazi Chelsea baada ya kuwa hapo kwa Miezi minane tu.

Tottenham ilipigwa Bao 6-0 na Man City hapo Novemba 24 na, ingawa walitoka Droo na Mabingwa Man United na kuzifunga Fulham na Sunderland, kipigo hiki cha Liverpool kimewachukiza Wamiliki wa Klabu hiyo ambayo mwanzoni mwa Msimu ilimuuza Gareth Bale kwa Dau la Pauni Milioni 85 kwa Real Madrid, ikiwa ni Rekodi ya Dunia, na kununua msululu wa Wachezaji ambao ni Paulinho, Roberto Soldado, Nacer Chadli, Etienne Capoue, Christian Eriksen, Vlad Chiriches na Erik Lamela lakini Timu imekuwa ikifanya vibaya kwenye Ligi.

Hata hivyo, kwenye michuano ya Ulaya ya EUROPA LIGI, Tottenham imekuwa ikifanya vyema na kushinda Mechi zao zote 6 za Kundi lake na kutinga Raundi ya Mtoano ya Timu 32 ambako leo wamepangiwa kucheza na Dnipro, Klabu ya Ukraine.

Mbali ya mafanikio hayo, Villas-Boas pia ameipeleka Tottenham kwenye Robo Fainali ya Capital One Cup ambako Desemba 8 watacheza na West Ham.

Villas- Boas anakuwa Meneja wa 5 Msimu huu kutimuliwa kazi toka Klabu ya Ligi Kuu England wengine wakiwa Steve Clarke, aliefukuzwa Jana kutoka West Bromwich Albion, pamoja na Paolo Di Canio aliefukuzwa Sunderland Mwezi Septemba, Ian Holloway alitimuliwa Crystal Palace Mwezi Oktoba na Martin Jol aliepoteza kazi Fulham Wiki 2 zilizopita.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad