![]() |
Watu wapatao
4,500 wakiwemo wawakilishi wa mataifa mbalimbali wamehudhuria mazishi hayo.
|
![]() |
"Kamera
hazikuruhusiwa wakati wa mazishi, familia haikutaka watu waone maiti ilipoteremshwa
kaburini," wala Vyombo vya habari na wageni wa hishima hawakuweza
kuhudhuria pia.
|
Akihutubia
maelfu ya watu waliofika kuhudhuria mazishi ya Mandela, Rais wa Afrika Kusini
Jacob Zuma amewataka wananchi wake kuendeleza urithi mwema walioachiwa na
kiongozi huyo.
Watu
mbalimbali waliopata fursa ya kuhutubia waombolezaji wameeleza wasifu wa
kiongozi huyo, huku Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akibainisha jinsi
uhusiano baina ya Mataifa hayo mawili ulivyoimarishwa na waasisi wa Mataifa
hayo, Hayati Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mandela ambao kwa pamoja
wanakumbukwa kwa harakati zao katika historia ya ukombozi barani Afrika.
![]() |
"Kamera hazikuruhusiwa wakati wa mazishi, familia haikutaka watu waone maiti ilipoteremshwa kaburini," wala Vyombo vya habari na wageni wa hishima hawakuweza kuhudhuria pia. |
No comments:
Post a Comment