Taswira ya Mazishi ya Nelson Mandela katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Eastern Cape . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 15, 2013

Taswira ya Mazishi ya Nelson Mandela katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Eastern Cape .

Mazishi ya Nelson Mandela yanaendelea leo (Desemba 15,2013) katika kijiji cha Qunu katika mkoa wa Eastern Cape na kumaliza wiki moja ya maombolezi ya shujaa wa Afrika mwendazake Nelson Mandela.


Wanajeshi hawa walisindikiza jeneza la Mandela hadi katika ukumbi maalum ambako ibada ya kumuaga Mandela ilifanyika .


Waliokuwa wake za Mandela walikesha usiku kucha kabla mazishi kufanyika leo()Desemba 15,2013).

Ngozi iliyofunikwa jeneza la Mandela kama ishara ya umuhimu wa Mandela katika jamii ya watu wa Thembu.

Kuambatana na tamaduni za watu wa Thembu ukoo wa Mandela, jeneza la mfu hufunikwa kwa ngozi ya Ng'ombe ishara ya umuhimu wake katika jamii.

Wageni mashuhuri walifika hapa kumuaga Mandela akiwemo Oprah Winfrey na Richard Branson na wengi wangineo.


Takriban watu 4,500 ikiwemo wageni wa kimataifa wanahudhuria mazishi hayo ambayo ni ya mchanganyiko wa tamaduni za kale na mambo ya kisasa.

Familia ya Mandela ilikesha wakijiandaa kwa mazishi ya leo huku kukiwa na muimbaji ambaye atakuwa anaita mizimu ya mababu wa kale na pia wakiongelesha mwili wa Mandela kumwambia kuwa sasa anazikwa. 

Ni kuambatana na tamaduni na mila za watu wa ukoo wa Mandela wa Thembu

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad