Boxing Day football - Arsenal, Chelsea & Manchester United zashinda Ligi Kuu Uingereza sasa Arsenal Kileleni na pointi 39. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, December 26, 2013

Boxing Day football - Arsenal, Chelsea & Manchester United zashinda Ligi Kuu Uingereza sasa Arsenal Kileleni na pointi 39.

Klabu ya Manchester United imetoka nyuma kwa mabao mawili na kushinda 3-2 dhidi ya Hull City katika Uwanja wa KC, huku James Chester, Mchezaji alieanzia Soka lake huko Old Trafford, ameifanya Man United ishinde mchezo huo baada ya kujifunga mwenyewe Bao la 3 katika Dakika ya 66.


Chester ndie alieipa Hull Bao la kuongoza na ndani ya Dakika 13 waliongoza Bao 2-0 baada ya Shuti hafifu la David Meyler kumbabatiza Jonny Evans na kumhadaa Kipa De Gea.

Lakini Man United walizinduka na Chris Smalling kuunganisha kwa kichwa frikiki nzuri ya Wayne Rooney na kufunga Goli la Kwanza na Dakika 7 baadae Wayne Rooney aliisawazishia Man United kwa Bao tamu baada kusogezewa na Danny Welbeck.

Hilo ni Bao la 150 kwa Rooney kwenye Mechi za Ligi akiwa na Man United na kumfanya awe Mechezaji wa Pili kufikisha idadi hiyo akichezea Klabu moja tu na mwingine ni Thiierry Henry aliekuwa Arsenal na kufunga Bao 175.

Hadi Haftaimu Bao zilikuwa 2-2 na ndipo Kipindi cha Pili Chester alipojifunga kwa kichwa baada kuicheza krosi ya Ashley Young iliyokuwa ikielekea kwa Rooney.

Valencia alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu kwenye Dakika ya 90 baada kupewa Kadi ya Njano ya Pili kwa kupoteza muda kwa makusudi.

Latest Football

As It Stands Table


Position Team Played Goal Difference Points
1 Arsenal 18 18 39
2 Chelsea 18 15 37
3 Liverpool 17 23 36
4 Man City 17 31 35
5 Everton 18 12 34
6 Newcastle 18 6 33
7 Man Utd 18 9 31
8 Tottenham 18 -5 31
9 Southampton 18 7 27
10 Stoke 18 -8 21
11 Swansea 18 -1 20
12 Hull 18 -7 20
13 Aston Villa 18 -7 19
14 Norwich 18 -15 19
15 West Brom 18 -5 17
16 Cardiff 18 -15 17
17 Crystal Palace 18 -15 16
18 Fulham 18 -16 16
19 West Ham 18 -10 14
20 Sunderland 18 -17 13

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad