Mgombea Ubunge Jimbo la Ngara 2010,Dk Peter Bujari atangaza rasmi kujiunga na Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, December 27, 2013

Mgombea Ubunge Jimbo la Ngara 2010,Dk Peter Bujari atangaza rasmi kujiunga na Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA.


Dk Peter Bujari.( Picha kutoka Maktaba) alijiunga na CCM mwaka 1995 na amekuwa akijuhusisha na utoaji wa huduma za kijamii hasa elimu na afya katika wilaya ya Ngara kupitia shirika lake la HUMAN DEVELOPMENT TRUST (HDT) ambapo amesaidia kuhamasisha jamii kuondokana na magonjwa ya malaria na  kusaidia jamii zenye uwezo duni.


Aliyekuwa mgombea Ubunge Jimbo la Ngara mkoani Kagera,kupitia Chama cha Mapinduzi CCM katika uchaguzi mkuu uliopita 2010 ,Dk. Peter Bujari ametangaza rasmi kukihama chama chake na kujiunga na chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA.

Akizungumza na wandishi wa habari nyumbani kwake katika kijiji cha Bikiriro wilayani Ngara,Dk Bujari alisema ameamua kujiunga na CHADEMA baada ya kuridhishwa na sera na uwajibikaji ndani ya chama hicho.

Alisema kuwa atakabidhi kadi ya CCM kwa Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Bw. Freeman Mbowe ambaye anatarajiwa kuwa wilayani Ngara Jumamosi Disemba 28 mwaka huu.

Awali taarifa kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA Bw. Stanford Kennedy Festo zililidokeza  kuwa Dk. Bujari alikuwa na mpango wa kuhamia CHADEMA na kwamba suala hilo lingetangazwa rasmi baadae.

Hata hivyo alisema kuondoka kwake CCM na kwenda CHADEMA ni kutaka kuleta mabadiliko katika upinzani dhidi ya Chama cha Mapinduzi, na kwamba atahakikisha kuwa wafuasi aliokuwa nao wanahamia kwenye chama hicho.

Dk Bujari alisema Chama cha Mapinduzi CCM kina muda mrefu tangu kuanzishwa kwake lakini kimeshindwa kuwajibika na kuwaletea maendeleo wananchi hali ambayo yeye kama mzalendo hawezi kuivumilia.



Dk Peter Bujari alijiunga na CCM mwaka 1995 na amekuwa akijuhusisha na utoaji wa huduma za kijamii hasa elimu na afya katika wilaya ya Ngara kupitia shirika lake la HUMAN DEVELOPMENT TRUST (HDT) ambapo amesaidia kuhamasisha jamii kuondokana na magonjwa ya malaria na  kusaidia jamii zenye uwezo duni.


Pamoja na jitihada zake ametoa msaada kwa watoto yatima kuwaendeleza kielimu katika wilaya za Ngara na Biharamulo huku baadhi ya familia zikipewa mitaji ya fedha ama mifugo (mbuzi kuendeleza maisha na kuongeza kipato cha familia.

Mwaka 2010 alikuwa kwenye orodha ya  wanachama 10 wa CCM waliowania  nafasi ya ubunge  kwenye jimbo la uchaguzi la Ngara ambapo wanachama  walimpa kura 2713 na aliyepata nafasi hiyo ni Mbunge wa sasa kupitia chama hicho Deogratias Ntukamazina aliyepata kura  4900 za wanachama wa CCM.
 
Source:-Ngara kwetu blog.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad