Arsenal yavutwa na Everton katika Ligi (EPL) huku UEFA Jumatano wakingoja uhakika wa kufuzu kwa matokeo ya Mechi yao ya mwisho Ugenini huko Italia dhidi ya Napoli. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 09, 2013

Arsenal yavutwa na Everton katika Ligi (EPL) huku UEFA Jumatano wakingoja uhakika wa kufuzu kwa matokeo ya Mechi yao ya mwisho Ugenini huko Italia dhidi ya Napoli.


Mchezaji Mesuit Ozil akishangilia na wachezaji wenzake wa Arsenal baada ya kufunga bao.Sasa, Arsenal wapo juu kwenye Msimamo wa Ligi ya Uingereza wakiwa Pointi 5 mbele ya Liverpool na Chelsea.


Mesut Ozil akiifungia Arsenal bao la kuongoza katika dakika ya 80 ya mchezo.

Gerard Deulofeu wa Everton (kushoto) akishangilia bao la kusawazisha dakika ya 81 ya mchezo.

Beki wa Arsenal Laurent Koscielny (kushoto) akijaribu kumzuia Steven Pienaar wa Everton wakati wa mchezo huo.


Vinara wa Ligi Kuu Uingereza , Arsenal jana (Desemba 08,2013)  wamekatwa makali yao ya kuzidi kuchanja mbuga kileleni baada kwenda Sare ya Bao 1-1 na Everton Uwanjani Emirates.

Sasa, Arsenal wapo juu kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa Pointi 5 mbele ya Liverpool na Chelsea.



Position Team Played Goal Difference Points
1 Arsenal 15 19 35
2 Liverpool 15 16 30
3 Chelsea 15 13 30
4 Man City 15 26 29
5 Everton 15 9 28
6 Tottenham 15 -1 27
7 Newcastle 15 -1 26
8 Southampton 15 5 23
9 Man Utd 15 3 22
10 Aston Villa 15 -2 19
11 Swansea 14 1 18
12 Stoke 15 -5 17
13 Hull 14 -6 17
14 Norwich 15 -14 17
15 West Brom 15 -4 15
16 Cardiff 15 -11 14
17 West Ham 15 -6 13
18 Fulham 15 -12 13
19 Crystal Palace 15 -12 13
20 Sunderland 15 -18 8

Hadi Mapumziko, Timu hizi zilikuwa Droo 0-0 na zikiwa zimebaki takriban Dakika 20, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, aliamua kuingiza Wachezaji watatu kwa mpigo, Mathieu Flamini, Tomas Rosicky na Theo Walcott na kuwatoa Santi Cazorla, Aaron Ramsey na Jack Wilshere.

Mabadiliko hayo yalileta uhai na katika Dakika ya 80 Tomas Rosicky alipiga krosi iliyomkuta Theo Walcott ambae nae krosi yake ilishindwa kuunganishwa na Olivier Giroud na kumdondokea Mesut Ozil aliefunga Bao kwa Arsenal.

Bao hilo lilidumu Dakika 4 tu kwani Chipukizi alietoka kwa Mkopo Barcelona, Gerard Deulofeu, mwenye Miaka 19, na alietokea Benchi kuchukua nafasi ya Kevin Mirallas, alimalizia kazi njema ya Chipukizi mwingine, Ross Barkley, iliyoshindwa kuunganishwa na Romelu Lukaku baada kuukosa Mpira kwa tikitaka, na kumkuta Deulofeu aliepiga kifundi na kucheka na kamba.


Wenger encouraged
 by Everton draw.
Arsenal wangeweza kuibuka kidedea kwani katika Dakika ya 93, Dakika ya mwisho ya muda wa Nyongeza wa Dakika 3, Olivier Giroud aliachia mzinga wa Mita 25 uliopiga besera.


Arsenal, licha ya kushinda Mechi 4 kati ya 5 katika Kundi F la UEFA, bado wanangoja uhakika kwa matokeo ya Mechi yao ya mwisho Ugenini huko Italy na Napoli.

Aidha Michuano ya Vilabu Ulaya  UEFA , hatua ya Makundi inafikia tamati  Jumanne na Jumatano, kwa Mechi za mwisho na tayari Timu 8 zimejihakikishia kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 na bado zipo Nafasi 8.

Timu 8 zilizofuzu ni Mabingwa Watetezi Bayern Munich, Chelsea, Manchester City, Manchester United, Real Madrid, Paris St-Germain, Barcelona, na Atletico Madrid.


MECHI ZA MWISHO ZA MAKUNDI
[SAA 4 Dakika 45 Usiku]
Jumanne 10 Desemba 2013.

Manchester United FC v FC Shakhtar Donetsk
Real Sociedad de Fútbol v Bayer 04 Leverkusen
Galatasaray v A.Åž. Juventus
FC København v Real Madrid CF
SL Benfica v Paris Saint-Germain
Olympiacos v FC RSC Anderlecht
FC Bayern München v Manchester City FC
FC Viktoria Plzeň v PFC CSKA Moskva

Jumatano 11 Desemba 2013

FC Schalke 04 v FC Basel 1893
Chelsea FC v FC Steaua BucureÅŸti
Olympique de Marseille v Borussia Dortmund
SSC Napoli v Arsenal FC
FK Austria Wien v Football Club Zenit
Club Atlético de Madrid v FC Porto
AC Milan v AFC Ajax
FC Barcelona v Celtic FC

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad