Gari aina ya
ya lsuzu lenye namba za usajili T 749 CCG baada ya kupata ajali eneo la Mindu
mkoani Morogoro - (Picha /
Habari na Dustan Shekidele GPL, Morogoro).
|
Gari aina ya
ya lsuzu lenye namba za usajili T 749 CCG baada ya kupata ajali eneo la Mindu
mkoani Morogoro - (Picha /
Habari na Dustan Shekidele GPL, Morogoro).
|
GARI aina ya
Isuzu yenye namba za usajili T749 CCG lililokuwa likisafirisha nyanya kutoka
kijiji cha Mlali kuelekea kwenye moja ya masoko ya mji wa Morogoro jana (Julai 31,2013) mchana
lilipata ajali na kupinduka eneo la Mindu jirani na bwawa la Mindu mkoani Morogoro.
Mashuhuda wa
tukio hilo walidai kwamba gari hilo lilipinduka baada ya kujaribu kumkwepa
mwendesha bodaboda na kwamba katika ajali hiyo hakuna mtu aliyepoteza maisha
ingawa baadhi ya wamiliki wa mizigo iliyokuwemo katika gari hilo walijeruhiwa.
'Unajua hivi
vigari ni vyepesi sana hivyo kikiyumba kidogo tu kinapinduka, wafanyabiashara
kwa kawaida huwa wanakaa juu ya matenga yao lakini kwenye tukio hili wamiliki
wa matenga hayo ya nyanya walikaa kwa dereva, sipati picha kama wangekaa juu ya
matenga yao kama ilivyozoeleka siku zote" alisema shuhuda huyo
aliyejitambulisha kwa jina la Johnson Joseph.
No comments:
Post a Comment