Kikosi cha
timu ya taifa ya Uganda 'Uganda Cranes' ndicho kilichoiburuza Taifa Starz na
kwa mabao 3-1 na hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 4-1.
|
Mchezaji wa Taifa Stars Aggrey Morris
(katikati) akiwania mpira huku akizongwa na mabeki wa Uganda Cranes.Taifa Stars
inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
|
Amri Kiemba akipongezwa na Mrisho Ngasa/
Aboubakar Salum 'Sure Boy' baada ya kushinda bao la kusawazisha dhidi ya Uganda
Cranes.
|
Washabiki wa Taifa Stars wakishangilia goli la
kusawazisha. Lililofungwa na...Amri Kiemba dhidi ya Uganda Cranes.
|
Amri Kiemba dhidi ya Uganda Cranes. |
Timu
ambazo zitacheza Fainali za CHAN mwaka 2014
huko nchini Afrika Kusini kuanzia
Januari 10 Mwakani zimefikia 9 na kubakia 7, baada ya Timu kadhaa kufuzu jana Jumamosi
(Julai 27,2013) .
Leo
(Julai 28,2013), Timu nyingine 3 zitafuzu na Congo-Brazzaville, Mali na Sudan
zipo kwenye nafasi nzuri kuchukua nafasi hizo wakati Sudan wakirudiana na
Burundi huko Khartoum baada ya kutoka sare 1-1 katika Mechi ya kwanza, Congo
wakirudiana na Congo DR huku Mali, walioshinda Mechi ya kwanza 3-1, wakicheza
ugenini na Guinea.
Zambia
noa wapo kwenye hali nzuri kutinga Fainali baada ya Jana kutoka Sare ugenini ya
Bao 1-1 na Botswana.
Timu
zilizofuzu hapo Jana :-
-South
Africa [Wenyeji]
-Libya
-Morocco
-Mauritania
-Ghana
-Nigeria
-Burkina
Faso
-Ethiopia
-Uganda
Tanzania (Taifa Stars) ilishindwa kufuzu Fainali za
Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) kwa mara ya pili mfululizo baada ya jana
(Julai 27 mwaka huu) kufungwa mabao 3-1 na Uganda Cranes, hivyo kutolewa kwa
jumla ya mabao 4-1.
Stars ambayo ilicheza fainali za kwanza
zilizofanyika Ivory Coast mwaka 2009 ilimaliza kipindi cha kwanza katika mechi
hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya
Kampala ikiwa sare ya bao 1-1.
Wenyeji ndiyo walioanza kufunga bao dakika ya saba
katika mechi hiyo iliyochezeshwa na Kanoso Abdoul Ohabee kutoka Madagascar.
Frank Kalanda alifunga bao hilo akimalizia mpira
uliopigwa ndani ya eneo la hatari la Tanzania.
Bao hilo halikuonekana kuichangaza Taifa Stars,
kwani ilitulia na kufanikiwa kusawazisha dakika ya 18 mfungaji akiwa Amri
Kiemba kutokana na pasi nzuri ya Mrisho Ngasa kwenye kona ya eneo la mita 18.
Dakika ya 32 nusura Taifa Stars ipate bao, lakini
mkwaju maridadi wa Mrisho Ngasa ambao tayari ulikuwa umempira kipa HAmza
Muwonge uligonga mwamba kabla ya kuokolewa na mabeki wa Uganda Cranes.
Mabao mengine ya Uganda Cranes yalifungwa dakika ya
48 kupitia kwa Brian Majwega na lingine dakika ya 63 mfungaji akiwa tenda
Kalanda kutokana na makosa ya Salum Abubakar kupokonywa mpira wakati akiwa
katika nafasi nzuri ya kutoa pasi kwa mwenzake.
No comments:
Post a Comment