Ni muonekano wa Kivuko cha zamani kilichokuwa kikitumiwa na Wananchi wa Ngara
kuvuka mto Ruvubu.
|
Wananchi wakimshangilia Rais Kikwete baada ya
kuzindua kivuko cha MV Ruvuvu jana Jumamosi (Julai 27,2013).
|
Rais Kikwete akishiriki kupiga ngoma na
kikundi cha utamaduni cha Ngara wakati wa uzinduzi wa kivuko cha MV Ruvuvu
katika mto Ruvubu wilayani Ngara mkoani Kagera.
|
Ni muonekano wa Umati wa Watu ukimsikikliza
Rais Kikwete akiwahutubia kwenye mkutano
wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Rulenge,Wilayani Ngara mkoani Kagera.
|
Rais Kikwete akisimikwa kuwa chifu wa Wahaya
na kukakabidhiwa mgolole na silaha za jadi za Wahaya katika sherehe ya kuzindua
wilaya mpya ya Kyerwa.
|
Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi
wa wilaya mpya ya Kyerwa wakati Rais Jakaya Kikwete alipokuwa mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya
siku sita.
|
Umati uliojitokeza katika sherehe za uzinduzi
wa wilaya mpya ya Kyerwa wakati Rais Jakaya Kikwete alipokuwa mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya
siku sita.
|
Waziri wa Ardhi Profesa Anna Tibaijuka
akishiriki katika ngoma ya utamaduni wakati wa mapokezi ya Rais Kikwete
wilayani Muleba mkoani Kagera.
|
Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wageni wakati ziara yake ya siku sita Mkoani Kagera.
|
Wananchi wa Muleba wakimshangilia Rais Jakaya
Mrisho Kikwete alipowasili wilayani humo akiwa katika ziara yake ya siku sita
Mkoani Kagera.
|
Rais Kikwete akimtwisha ndoo ya maji mmoja wa Wananchi wa Muleba baada ya kuzindua mradi mkubwa wa maji kwa wilaya hiyo.
|
Vikundi vya ngoma vikitumbuiza wageni wakati ziara yake ya siku sita Mkoani Kagera.
|
Rais Kikwete akijiunga na waumini wa wilaya ya Muleba
kusali swala ya Magharibi kabla ya kufuturu wakati huu Waislam Duniani wakiwa katika Mfungo wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.
|
Dua ikisomwa baada ya futari aliyoandaa Rais
Kikwete kwa wananchi wa Muleba.
|
Rais Kikwete akisalimia wananchi akiwa katika
ziara yake ya siku sita Mkoani Kagera.
|
No comments:
Post a Comment