Kushoto
ni Padre Johnbosco mhasibu wa jimbo la Rulenge-Ngara akiwa na Paroko wa
Rwinyana Padre Patrick Kalile wakielekea kutabaruku makaburi katika misa ya
shukrani ya Ansigar Patrick kaisile.
|
Kushoto
ndiye Padre Kataisile akiwa na Mwenzake kutoka Songea.
|
Mapadre
wa Parokia ya Rulenge na Rwinyana na waliotoka Peramiho songea wakisali kwa
pamoja katika ibada ya shukrani kwa Padre Ansigar baada ya kupata daraja la
upadre may 30 mwaka huu huko Songea.
|
Masister
wa Nyabihanga parokia ya Rwinyana na waumini wa parokia hiyo wakiwa katika
ibada ya kutabaruku makaburi ya familia ya padre Asigar Kaisile nyumbani kwao
Kilinzi Rwinyana Ngara.
|
Mbunge
wa Ngara akiwa na mwl Ghaitani Francis Nturo ( kaka yake padre Ansigar ) pamoja
na masister wakiwa katika ibada ya kutabaruku makaburi baada ya misa ya
shukrani.
|
Vijana
wa rika na madhehebu mbali mbali wametolewa rai ya kuwa na uvumilivu katika harakati za kukabiliana
na changamoto za maisha zikiwemo za miito mitakatifu mbele za Mungu.
Wito
huo umetolewa jumapili ya wiki iliyopita na Padre Ansigar Patrick kaisile
kutoka Peramiho ya songea mkoani Ruvuma wakati wa misa ya shukrani katika
parokia ya Rinyana jimbo katoliki la Rulenge Ngara baada ya kupata daraja hilo
miaka 38 iliyopita.
Padri
kaisile akiongea na kipindi hiki muda mfupi mara baada ya sherehe za shukrani
katika Parokia ya Rwinyana wilayani Ngara amesema kuwa vijana wengi wanashindwa
kutimiza malengo yao kwa kukosa uvumilivu na kushindwa mitihani katika maisha
yao.
Amesema
kuwa vijana wajitokeze katika miito ya
kumtumikia mungu kwa kujiunga na mashirika ya kitume na kujifunza maadili ya
kiroho na fani mbalimbali
zitakazowasaidia kulipa fadhira kwa wazazi na jamii wanakozaliwa au kutumikia
katika kueneza neon la Mungu.
Aidha
amewashukuru waliofanikisha yeye kupata daraja la upadre tangu aanze kuweka
nadhiri tangu mwaka 1978 wakiwemo walimu
wa dini shule ya msingi na sekondari pamoja na mashirika yaliyomuongezea ujuzi
akiwa Afrika ya kusini kusomea utaalamu katika nishati ya umeme.
Kwa
upande wake Padre Angelo Msele kutoka shirika la Mtakatifu Benedicto lililoko
peramiho wilayani songea mkoani Ruvuma katika kuzungumza na kipindi hiki
amesema wazazi wanalo jukumu la kupeleka watoto wao katika shule za elimu zenye
mafunzo ya kiroho kuwajengea nidhamu
katika maisha yao.
No comments:
Post a Comment