|
Majeneza yenye miili ya Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania
(JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini Sudan Julai 13, 2013 kutokana
na shambulizi la ghafla, yakiwa eneo la tukio tayari kuagwa leo(Julai 22,2013)
katika Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Rais Jakaya Kikwete, mkewe Mama Salma, wakitoa
heshima za mwisho mbele ya majeneza yenye miili ya Askari wa Jeshi la Ulinzi la
Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini Sudan
Julai 13, 2013 kutokana na shambulizi la ghafla, wakati wa zoezi la kutoka
heshima zao za mwisho kuaga miili ya askari hao leo katika Uwanja wa Wizara ya
Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za mwisho mbele ya majeneza yenye
miili ya Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza
maisha Jimboni Darfur nchini Sudan Julai 13, 2013 kutokana na shambulizi la
ghafla, wakati wa zoezi la kutoka heshima zao za mwisho kuaga miili ya askari
hao leo(Julai 22,2013) katika Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya
Kikwete, akitia saini katika Kitabu cha Maombolezo ya Askari wa Jeshi la Ulinzi
la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini Sudan
kutokana na shambulizi la ghafla, wakati Rais na viobgozi wengine walipofika
kutoka heshima zao za mwisho kuaga miili ya askari hao leo (Julai 22,2013) katika Uwanja wa
Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Makamu wa Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika Kitabu cha Maombolezo ya Askari
wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni
Darfur nchini Sudan kutokana na shambulizi la ghafla, wakati Makamu na viobgozi
wengine walipofika kutoka heshima zao za mwisho kuaga miili ya askari hao leo(Julai 22,2013)
katika Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, akitia saini katika
Kitabu cha Maombolezo ya Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania
(JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini Sudan kutokana na shambulizi la
ghafla, wakati walipofika kutoka heshima zao za mwisho kuaga miili ya askari
hao leo(Julai 22,2013) katika Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji wafiwa baada ya kutoa heshima za mwisho
kwa miili ya Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini Sudan Julai 13, 2013 kutokana na
shambulizi la ghafla, wakati wa zoezi la kutoka heshima zao za mwisho kuaga
miili ya askari hao leo(Julai 22,2013) katika Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es
Salaam.
|
|
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Idd,
akiwafariji wafiwa baada ya kutoa heshima za mwisho kwa miili ya Askari wa
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni
Darfur nchini Sudan Julai 13, 2013 kutokana na shambulizi la ghafla, wakati wa
zoezi la kutoka heshima zao za mwisho kuaga miili ya askari hao leo katika
Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga jijini Dar es Salaam.
|
|
Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Regnard Mengi, akiwa
na baadhi ya viongozi, wakitoa heshima za mwisho mbele ya Majeneza yenye miili
ya Askari wa kulinda Amani, wa jeshi la Ulinzi la Tanzania, waliokufa huko
Darfur Julai 13, 2013, wakati wa zoezi la kuagwa miili hiyo lililofanyika leo
(Julai 22,2013) kwenye Uwanja wa Wizara ya Ulinzi, Upanga jijini Dar.
|
|
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake, Dkt. Bilal, na
viongozi wengine wakiwa katika shughuli hiyo ya kuagwa miili ya askari hao leo
(Julai 22,2013) kwenye Uwanja wa Wizara ya Ulinzi Upanga Dar es Salaam.
|
|
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, John Nchimbi
akiteta jambo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard
Membe, wakati wakiwa katika shughuli hiyo ya kuaga miili ya Askari wa Jeshi la
Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliopoteza maisha Jimboni Darfur nchini
Sudan kutokana na shambulizi la ghafla. Kulia ni Katibu wa CCM, Abdulrahman
Kinana.
|
|
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza wakati wa
zoezi hilo leo(Julai 22,2013) la kuiaga miili saba ya wanajeshi wa jeshi la wananchi wa Tanzania
waliouwawa nchini Sudan Jumamosi ya July 13 mwaka huu.
|
|
Mkuu wa Majeshi,Jenerali Davis Mwamunyange,
akizungumza wakati wa zoezi hilo la kuiaga miili saba ya wanajeshi wa jeshi la
wananchi wa Tanzania waliouwawa nchini Sudan Jumamosi ya July 13 mwaka huu.
|
|
Baadhi ya wafiwa wakiwa na huzuni huku wengine
wakilia kwa uchungu wakati wa kuagwa miili hiyo leo(Julai 22,2013).
|
|
Baadhi ya wafiwa wakiwa na huzuni huku wengine
wakilia kwa uchungu wakati wa kuagwa miili hiyo.
|
|
Baadhi ya Askari pia wakiwa na nyuso za huzuni.Picha na:Ofisi ya OMR.
|
Amirjeshi
mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Rais Jakaya Kikwete akiongozana na
viongozi mbalimbali waandamizi katika serikali ya Jamhuri ya Muungano na
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na watu maarufu amewaongoza mamia ya
waombolezaji katika kuiaga miili saba ya wanajeshi wa jeshi la wananchi wa
Tanzania waliouwawa nchini Sudan Jumamosi ya July 13 mwaka huu.
Dr
Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza katika viwanja vya makao makuu ya jeshi hilo
akionekana dhahiri shairi mwenye majonzi ikiwa ni muda mfupi mara baada
ya kuwaongoza mamia ya waombolezaji kuiaga miili ya wanajeshi hao waliouwawa na
kikundi cha waasi nchini Sudan katika jimbo la Darfur amesema taarifa za tukio
hilo limemuhuzunisha,kumsikitisha na kumkasirisha na kushauri kuwa wakati
umefika wa kuutazama upya mfumo mzima wa kulinda amani Darfur hasa kuhusu
kiwango cha uwezo wa wanajeshi kujilinda kutokana na ukweli kuwa tayari walinda
amani 41 kutoka mataifa mbalimbali wameuwawa na wengine 55 kujeruhiwa.
Aidha
waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa Mh Shamsi Vuai Nahodha amekiita
kitendo cha wanajeshi hao wakulinda amani kuuwawa ni dhahiri tendo ovu ambao ni
mkakati maalum wa waasi kutaka kuhakikisha mpango wa umoja wa mataifa katika
kuleta amani katika nchi zenye mifarakano hazifanikiwi huku salamu za rais wa mapinduzi
ya Zanzibar Dr Ally Mohamed Shein zikisomwa na mwakilishi.
Mkuu
wa majeshi ya ulinzi hapa nchini jenerali Davis Mwamunyange amesema wanajeshi
hao walishambuliwa na waasi wakati wakisindikiza na kutoa ulinzi kwa waangalizi
wa amani na washauri wa polisi na kwamba walipopunguza mwendo kutokana na
utelezi uliosababishwa na mvua umbali wa kilomita 25 kutoka Darfur ndipo
waliposhambuliwa.
Zoezi
hilo la kuiaga miili ya mashujaa hao waliouwawa nchini Sudan mbali na
kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali waandamizi serikalini pia limehudhuriwa na
watu mbalimbali maarufu akiwemo mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya IPP Dr
Regnald Mengi huku aliyekuwa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa Dr Asha Rose
Migiro akisema tukio hilo lisiwakatishe tamaa katika kupigania amani ya watu
wengine katika nchi zenye mifarakano.
No comments:
Post a Comment