Maji yapungua eneo la Chipite na hali ya Usafiri katika wilaya za Mikoa ya Mtwara na Lindi japo kwa shida. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, April 10, 2013

Maji yapungua eneo la Chipite na hali ya Usafiri katika wilaya za Mikoa ya Mtwara na Lindi japo kwa shida.




Baada ya Maji kupungua katika eneo la Chipite ambalo lilijaa maji na  kusababisha Abiria zaidi ya 500 na Magari zaidi ya 200 kushindwa   kupita eneo hilo na Kufanya gari nyingi ziendazo na Kutoka Mtwara,Masasi,Ruangwa,Liwale,Nachingwea,Liwale,Nanyumbu na Tunduru na  kufanya safari kwa kuzunguka wilaya ya Newala sasa hali imeanza  kubadilika na gari nyingi kuanzia jioni zimeanza kupita ingawa kwa  Mashakamashaka ili kusaidia kupeleka na kutoa huduma kwa Jamii.





Kufuatia hali hiyo,Baadhi ya wasafiri waliokwama wametupia lawama kwa Wakala wa Barabara Tanroads na Kitengo cha Maafa kutotoa Ushiriakiano  wowote kuhakikisha Abiria wanakuwa salama ikiwa pamoja na  kutafuta jitihada za haraka kuwavusha ili kuepusha Maafa  yatakayochangiwa na uwepo wa msongamano kwa muda mrefu.





Hali ya usafiri sasa iko kama kawaida kuelekea katika wilaya Tajwa hapo Juu.


Picha na Mdau Abdulaziz Lindi.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad