Majerui wa Bomu Ngara,mkoani Kagera Wapelekwa KCMC. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, May 24, 2018

Majerui wa Bomu Ngara,mkoani Kagera Wapelekwa KCMC.

Watoto watatu waliojeruhiwa na Bomu katika Shule ya Msingi Kihinga wilaya ya Ngara mkoani Kagera Novemba 2017 wakiagwa   na Katibu Tawala wa wilaya hiyo Bw. Vedastus Tibaijuka (wa pili kushoto) wakielekea KCMC  kuwekewa macho bandia baada ya kampuni ya Kabanga Nickel kugharimia Shilingi milioni 4 za matibabu yao . 

Wa kwanza kushoto  ni Dkt Prosper Malya na wengine ni Wazazi wa Watoto hao wanaowasindikiza katika matibabu yao.

Wanafunzi hao  ni Emanuel Hilali , Domona Eliyuta na Veliana Isack  ambao wamesafiri chini ya mwangalizi Dkt. Prosper Malya nambapo  wawili kati yao watawekewa macho ya bandia kuepuka unyanyapaa kwa jamii inayowazunguka.
Mganga wa Hospitali ya Rulenge wilayani Ngara mkoani Kagera Dkt Prosper Malya  (kushoto) akiwasindikiza watoto watatu waliojeruhiwa na bomu katika shule ya msingi Kihinga wilayani  humo Novemba mwaka jana wakielekea KCMC  kuwekewa macho bandia baada ya kampuni ya Kabanga Nickel kugharimia Shilingi milioni 4 za matibabu yao hapo May 24, 2018. 

Picha Na Shaaban Ndyamukama.
Afisa Mahusiano  wa Kampuni ya Kabanga Nickel iliyoko wilaya ya Ngara mkoani Kagera Francis Wikedzi amesema kwamba Serikali  ya wilaya ilitoa maombi ya  kusaidia watoto hao  na kampuni kama sehemu ya Jamii imetafuta wahisani wa ndani na nje ya wilaya na kupata fedha za matibabu ya  watoto hao.

Amesema  fedha hizo zitatumika  kuwasafirisha watoto, wazazi wao na daktari mmoja kutoka Hospitali ya Rulenge pamoja na Dereva kwenda na kurudi ambapo pia zimeambatanishwa na gharama za matibabu kwa siku watakazoishi Hospitali ya KCMC.

Watoto watatu waliosafirishwa kwenda KCMC ni miongoni mwa majeruhi 42 wa bomu  la kutupwa kwa mkono katika shule ya msingi Kihinga wilayani Ngara Novemba 2017 na katika tukio hilo wanafunzi watano walipoteza maisha.
Januari mwaka huu (2018)  kampuni hiyo ilitoa msaada wa dawa zilizotumika kuwatibu majeruhi katika Hospitali ya Rulenge na kutoa pia vifaa vya kujifunzia na sare za wanafunzi 192 wa shule hiyo huku familia zilizopoteza  watoto watano zikipata ubani wa chakula vyote vikiwa na thamani ya Shilingi milioni 20.7.

Katibu tawala wa wilaya ya Ngara Vedastus Tibaijuka kwa niaba ya Serikali ametoa pongezi kwa Kampuni ya Kabanga Nickel kwa msaada huo na Taasisi ya Tumaini Fund  ambayo ilitoa Shilingi milioni 5 kuwatibisha  majeruhi waliotibiwa  Hospitali ya Kagondo wilayani Muleba kwa watoto watatu waliokuwa wamejeruhiwa miguu  yao.

Aidha Tibaijuka aliwashukuru pia Tumain Fund kwa kugharimia matibabu ya majeruhi 42 waliolazwa  Hospitali ya Rulenge na kushukuru jamii iliyoguswa na tukio hilo kwa kuchangia damu, mavazi vyakula na huduma nyinginezo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad