![]() |
Nahodha wa Simba John Bocco (kulia) akimkabidhi
kombe la ubingwa Mkurugenzi Mkuu wa SportPesa, Pavel Slavkov, huku viongozi
wengine kutoka Simba na kampuni hiyo wakishuhudia.
Akizungumza
kwenye hafla hiyo Kaimu Makamu wa Rais wa Simba, Iddi Kajuna, alisema
kuwa: “Tunaishukuru sana SportPesa kwa kututia nguvu
tangu mwanzo wa Ligi hadi leo hii ambapo wametukabidhi hundi hiyo ya
shilingi milioni 100, bila kujali hata kuwa bado tuna mchezo mmoja ili
tukamilishe ratiba yetu.
“Pia tunawashukuru SportPesa kwa kutuwezesha kulipa mishahara
ya wachezaji wetu mapema, jambo ambalo tunaamini kwa namna moja au nyingine
limechangia kwa kiasi kikubwa kwetu kuibuka mabingwa wa Tanzania kwani bila
kutoa mishahara kwa wakati yawezekana leo hii tusingeweza kufikia malengo
yetu,” alisema Kajuna.
|
![]() |
Baadhi ya wachezaji wa Simba SC na makocha wa timu
hiyo wakiwa ndani ya Ofisi za SportPesa.
|
![]() |
Wachezaji na viongiozi wa Simba SC na SportPesa
wakiwa katika picha ya pamoja.
|
![]() |
Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa,
Tarimba Abbas akizungumza jambo kabla ya makabidhiano ya hundi hiyo kufanyika Leo May 24,2018.
Naye
Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa SportPesa, Tarimba Abbas alisema: “Kwa
niaba ya kampuni yetu ya SportPesa nawapongeza sana Simba kwa kuwatendea haki
mashabiki wa Simba kwani kufanya hivyo mmetupa heshima kubwa sana sisi
wadhamini wenu wakuu, kwani mmeitendea haki sana nembo yetu kiasi cha kampuni
yetu kuamini kuwa imefanya jambo muhimu kuwa wadhamini wenu wakuu,” alisema Abbas.
|
![]() |
Kaimu Makamu wa Rais wa Simba SC Iddi Kajuna, akitoa
neno la shukurani.
|
No comments:
Post a Comment