Akizungumza
wakati wa zoezi la usafi March Mosi,2018, Mkurugenzi wa Radio Kwizera FM
Padre.Damas Missanga SJ, Aliwashauri wakazi wa Ngara na wageni kujiepusha na
utupaji wa taka ovyo, na kwamba suala la usafi ni la kila mtu na kwamba kwenye
kampeni ya usafi wao Wanaihamasisha Jamii,Viongozi mbalimbali na Mamlaka za
Usafi wilayani Ngara kutimiza wajibu wao katika kushiriki kwenye zoezi la usafi
wa mazingira mara kwa mara katika maeneo yao ili kuepukana na magonjwa
yatokanayo na uchafu kama vile kuhara na kipindupindu.
|
Uchunguzi wa
Radio Kwizera FM umebaini kwamba, katika maeneo ya Mji wa Ngara, mwitikio wa wananchi katika suala la usafi ni
mdogo mno huku wengi wao ameeleza kwamba, changamoto kubwa ni uchafu wa kudumu
kwenye maeneo ya Vizimba vya kutupia taka maeneo ambayo usafi wa mazingira
haufanyiki kama inavyotakiwa.
Kumbukumbu
zinaonyesha kwamba, katika kuhakikisha kampeni ya usafi wa mazingira kuwa ni ya
kitaifa na endelevu, mwaka 2015 na 2016 Rais Magufuli alilazimika kufuta baadhi
ya sherehe za kitaifa na kuzifanya kuwa siku za usafi kitaifa pamoja na
kuelekeza fedha kwenye upanuzi wa miundombinu.
|
No comments:
Post a Comment