Kutoka
kushoto ni Afisa Maendeleo ya Jamii wilayani Ngara mkoani Kagera Bw. Herman
Hume aliye muwakilisha Mkurugenzi Mtendaji katika mkutano huo, wapili ni Katibu
tawala wa wilaya ya Ngara,Bw.Vedastus Tibaijuka ,watatu ni Mwenyekiti CCM (W)
Bw. George Rubagora na wa nne ni Katibu CCM (W) Bi. Mwajemi Baragama.
Wajumbe hao
walisema kero kubwa ya wananchi ni kutokamilika miundombinu katika sekta hizo
kwa kujenga vyumba vya madarasa, nyumba za watumishi, zahanati na vituo vya
afya na kutatua migogoro ya ardhi baina
ya wakulima na wafugaji au wenye uwezo kifedha na maskini.
Mwenyekiti
wa CCM wilayani Ngara George Rubagora alisema miradi ya maji ya benki ya dunia
imekwama katika vijiji ilikoelekezwa na wanaoteseka ni wanafunzi, wazee, watoto
wadogo katika familia na wanawake kwa kutumia maji yasiyosafi na salama kisha
kuhatarisha afya zao.
Rubagora
alisema halmshauri haina budi kuongeza juhudi za kubuni vyanzo vipya vya mapato
na kuepuka kusubiria utozaji wa ushuru wa mazao kwa wafanyabiashara au walanguzi kwenye magulio na vibanda vya
ujasiriamali wanaotegemea mapato yao madogo kujikwamua kiuchumi.
"Ujenzi
wa miundombinu katika huduma za kijamii imefikia asilimia 34 kufikia Desemba
2017 na imekwama baada ya serikali kushindwa kutekeleza ilani ya chama tawala
na falsafa ya Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM taifa ya hapa kazi
tu" Alisema Rubagora.
|
Mjumbe
akichangia moja ya Hoja katika Kikao hicho.
Alisema
Halmashauri iliidhinishiwa na serikali kupata Sh 45.88 bilioni kwa mwaka
2017/2018 lakini fedha ambayo ilishapokelewa hadi Desemba 2017 ni Sh13
bilioni ambapo utekelezaji wa miradi iliyoibuliwa kiuhalisia iko chini ya malengo licha ya
uchangiaji wa vifaa kwenye maeneo yao
Kaimu Afisa
Mipango wa Halmashauri ya wilaya ya Ngara, Bw. Ghalibu Mkumbo alisema katika
bajeti ya mwaka 2017/ 2018 katika robo ya pili kufikia Desemba 31,2017 Halmashauri
hiyo ilikusanya Sh 520 milioni kati ya
Sh 2.03 bilioni kutoka vyanzo vya ndani na utekelezaji wa miradi mbalimbali
imefikia asilimia 34 kiuhalisia kisha kuwepo miradi mingi kubaki viporo
Hata hivyo
Mkumbo alisema halmashauri kwa fedha
zinazopatikana kutoka serikalini imeboresha miundombinu katika Sekta ya Afya
kwa kukarabati zahanati na vituo vya afya vyumba vya madarasa pamoja na barabara lakini changamoto ni fedha za utekelezaji wa miradi
ya maji ambayo imetelekezwa tangu kuanzishwa mwaka 2012.
“Katika mafanikio yaliyopo sekta ya
kilimo imejikita katika zao la biashara
la kahawa kwa kusambaza miche kwa wakulima huku idara ya mifugo iijihusisha na
upigaji chapa ng'ombe na kuchanja mifugo mingineyo kupunguza magonjwa
mbalimbali” Alisema Mkumbo.
|
Afisa Kilimo Costantine Mudende alisema
wilaya ya Ngara inayo mibuni ya kahawa 2,671,805 kati yake ni 1,113,960, ni aina ya arabika na 1557, 845 ni aina ya robusta, kwa wakulima wa kahawa 8,756 na kwamba idara
imesambaza miche 72,065 yenye thamani ya
Sh80 milioni katika kata 20 kutoka chuo
cha utafiti wa mazao cha Maruku mkoani Kagera
Kwa upande
wa Afisa mifugo Richard Ngowi alisema
jumla ya ng’ombe 68,713 katika vijiji 75 wamepigwa chapa kati ya ng'ombe
78,000 waliosajiliwa kwa wafugaji 5,197 ambapo idara ilikuwa imelenga kupiga
chapa ng'ombe 75,000
Pia alidai
kwamba kati ya January hadi December 2017 jumla ya Ng'ombe 886 walichanjwa
dhidi ya ugongwa wa ndigana kali katika kijiji cha Rwakalemela pia ng'ombe 12,239, walichanjwa dhidi ya
ugonjwa wa miguu na midomo, (FMD) katika
kijiji cha Kasulo.
|
Vile vile
alisema ng'ombe 2452 walichanjwa dhidi ya ugonjwa wa chambavu (BQ) na ng'ombe
4,167 walichanjwa dhidi ya homa ya mapafu (CBPP) Katika vijiji vya Rwakalemela
na Nyakariba kata ya Kasulo ambapo kuku
56, 058 walichanjwa dhidi ya ndondo na kuku 4532 walichanjwa dhidi ya ugonjwa
wa ndui katika mitaa ya Ngara mjini na kijiji cha Nyamiaga.
Hata hivyo
katibu tawala wa wilaya ya Ngara Vedastus Tibaijuka aliwataka wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM
kila kata kuhamasisha wananchi kuchangia miradi ya maendeleo wakati halmashauri
ya wilaya na serikali kwa ujumla ikitafuta vyanzo vya mapato kuboresha miundombinu ya kutoa huduma bora za kijamii.
|
No comments:
Post a Comment