Rais Magufuli na Uwekezaji Mpya Tanzania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, March 19, 2018

Rais Magufuli na Uwekezaji Mpya Tanzania.

Leo March 19, 2018 Moja ya shughuli inayoendelea ikulu ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli Ambae ni Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara ameongoza Mkutano wa 11 wa Baraza hilo.

Rais Magufuli ameuambia mkutano wa 11 wa Baraza la Biashara la Taifa kuwa ni Viwanda nane tu ikiwemo Kampuni ya Bakhresa ndivyo ambavyo vimekuwa havifanyi udanganyifu.

Rais John Magufuli leo Jumatatu, Machi 19 ameweka wazi matokeo ya kamati teule aliyoiunda kuchunguza mwenendo wa viwanda  vinavyoagiza sukari ya viwandani.
Rais Magufuli ameuambia mkutano wa 11 wa Baraza la Biashara la Taifa kuwa ni viwanda nane tu ikiwemo Kampuni ya Bakhresa ndivyo ambavyo vimekuwa havifanyi udanganyifu.

"Viwanda nane tu ndio safi, kuna baadhi ya viwanda vinakasoro ndogo ndogo ikiwemo kuagiza sukari nyingi zaidi ya mahitaji yao...lakini wapo wenye matatizo makubwa kabisa, vipo viwanda hewa kunakimoja kiliagiza tani 7,000 tukaambiwa kipo Mbeya kwenda huko hakikukutwa, ni kiwanda hewa, mi nilijua kuna wafanyakazi hewa tu, kumbe na viwanda pia vipo."

"Serikali yangu wala haina nia ya kuwasumbua wazalishaji wanaotumia sukari hii kihalali, lakini kwa mwenendo huu lazima tuwe macho ili sukari hii isiingie sokoni na kuumiza walaji."



Katika hatua nyingine,Rais John Magufuli ameeleza kuwa siku za hivi karibuni atakutana na Wakurugenzi Watendaji wawili kutoka nchi za Ujerumani na Denmark ambao watakuja kufanya uwekezaji nchini.

Rais Magufuli ameeleza kuwa watakuja kufanya uwekezaji wa kiwanda kipya cha Petroli Kemikali (Petrol Chemical Plant) ambacho kitakuwa na thamani ya Dola za Marekani Bilioni 1.92 ambayo ni sawa na takriban Shilingi za Kitanzania Trilioni 4.56.

Ameeleza kuwa kiwanda hicho kinatarajiwa kutoa ajira kwa Watanzania zaidi ya 4000 katika eneo la Kilwa kwa ajili ya kutengeneza mbolea ambayo itauzwa ndani pamoja na nje ya nchi kwa kutumia gesi iliyopo nchini.





No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad