Ngara/kagera- Ajichoma Moto Ndani ya nyumba baada ya Kumuua Mama Mkwe. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, March 17, 2018

Ngara/kagera- Ajichoma Moto Ndani ya nyumba baada ya Kumuua Mama Mkwe.

Muonekano wa nyumba ilivyoungua ndani eneo la tukio.

Kijana anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 32 mkazi wa kitongoji cha Nyakahanga kata ya Rusumo Wilayani Ngara Mkoani Kagera amejiua kwa kujichoma moto ndani ya nyumba baada ya kumuua Mama Mkwe wake pamoja na kumjeruhi Mke wake sehemu mbalimbali za mwili kwa kumchoma na kisu.

Tukio hilo limetokea majira ya saa 5 usiku wa kumkia leo March 17,2018 ambapo Bw Joseph Medadi amemuua Mama Mkwe wake Bi Elizabeth Simoth anaeyekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 na kisha kumjeruhi mke wake Elice Joseph anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 ambaye amelazwa katika hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara.
 


Mwili wa Marehemu eneo la tukio.

Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa kijiji cha Rusumo Bw Dauson Kadende amesema baada ya Bw Joseph Medadi kutekeleza tukio hilo ndipo akachukua uamuzi wa kujichoma moto ndani ya nyumba kwa kutumia petroli hali iliyosababisha kifo chake.
 


Nyumba ya Mama Mkwe ilivyoteketea kwa moto.

Kwa upande wake msemaji wa familia hiyo Bw Ezeckia Simion amesema chanzo cha tukio hilo ni kuwepo kwa  mgogoro wa kifamilia baina ya Marehemu Bw Joseph na Mke wake.
 

Juu na Chini Pichani ni Baadhi ya wakazi wa Nyakahanga kata ya Rusumo Wilayani Ngara Mkoani Kagera wakiwa eneo la tukio kufatilia na kufanya taratibu zinginezo.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Wilayani Ngara Bw Abeid Maige amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba upelelezi juu ya tukio hilo bado unaendelea.
 




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad