Muonekano wa nyumba ilivyoungua ndani eneo la tukio.
Kijana
anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 32 mkazi wa kitongoji cha Nyakahanga kata
ya Rusumo Wilayani Ngara Mkoani Kagera amejiua kwa kujichoma moto ndani ya
nyumba baada ya kumuua Mama Mkwe wake pamoja na kumjeruhi Mke wake sehemu
mbalimbali za mwili kwa kumchoma na kisu.
Tukio hilo
limetokea majira ya saa 5 usiku wa kumkia leo March 17,2018 ambapo Bw Joseph Medadi amemuua
Mama Mkwe wake Bi Elizabeth Simoth anaeyekadiriwa kuwa na umri wa miaka 70 na
kisha kumjeruhi mke wake Elice Joseph anaekadiriwa kuwa na umri wa miaka 28 ambaye
amelazwa katika hospitali ya Murugwanza wilayani Ngara.
|
Mwili wa Marehemu eneo la tukio.
Akizungumzia
tukio hilo, Mwenyekiti wa kijiji cha Rusumo Bw Dauson Kadende amesema baada ya
Bw Joseph Medadi kutekeleza tukio hilo ndipo akachukua uamuzi wa kujichoma moto
ndani ya nyumba kwa kutumia petroli hali iliyosababisha kifo chake.
|
Nyumba ya Mama Mkwe ilivyoteketea kwa moto.
Kwa upande
wake msemaji wa familia hiyo Bw Ezeckia Simion amesema chanzo cha tukio hilo ni
kuwepo kwa mgogoro wa kifamilia baina ya
Marehemu Bw Joseph na Mke wake.
|
Juu na Chini Pichani ni Baadhi ya
wakazi wa Nyakahanga kata ya Rusumo Wilayani Ngara Mkoani Kagera wakiwa eneo la
tukio kufatilia na kufanya taratibu zinginezo.
Mkuu wa
Jeshi la Polisi Wilayani Ngara Bw Abeid
Maige amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba upelelezi juu ya tukio
hilo bado unaendelea.
|
No comments:
Post a Comment