Naibu Waziri
wa Elimu William Ole Nasha jana March 1, 2018 alikuwa mkoani Mara
katika ziara ya kukagua ujenzi wa miundombinu ya shule inayoojengwa na Wizara
ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia programu ya lipa kulingana na
matokeo (EP4R).
Katika ziara
hiyo Ole Nasha ametoa onyo kwa walimu wote nchi wanaojihusisha
kimapenzi na wanafunzi na kuwaambia waache mara moja tabia ya kuwarubuni
wanafunzi badala yake warudishe nidhamu ya wanafunzi na kuinua kiwango cha
elimu na ufaulu katika shule wanazofundisha.
Ole Nasha
amesema amepokea taarifa juu ya baadhi ya walimu kujihusisha kimapenzi na
wanafunzi wao jambo ambalo ni kinyume cha sheria za nchi pamoja na maadili
ya utumishi wa umma.
Ameeleza
kuwa serikali haitamvumilia mwalimu yeyote mwenye tabia kama hizo na kuongeza
kuwa mwalimu atakayebainika kushiriki vitendo hivyo atashtakiwa kwa mujibu wa
sheria za nchi pamoja na kuchukuliwa hatua za kinidhamu kulingana na taratibu
za utumishi wa umma.
Pia
amewataka wazazi na walezi kuhakikisha hawajihusishi kwa namna yoyote kupokea
fedha ili kuwaficha wahalifu wanaokatiza masomo ya watoto wao kwa kuwapa ujauzito badala
yake waache sheria ichukue mkondo wake ili kusaidia kukomesha vitendo hivi viovu katika
jamii.
Nae Mkuu wa
wilaya ya ya Musoma Dk Vicent Naano amesema wilaya yake inakabiliwa na
tatizo la mimba za utotoni ambapo kwa mwaka wastani wa wanafunzi mia moja wanapata
ujauzito na kukatiza masomo.
|
No comments:
Post a Comment