Afisa Ustawi wa Jamii wilayani Ngara Musa Niyonsaba Balagondoza akiwa nyumbani kwa Babake na Anthony. |
Mwanafunzi
huyo Anthony Petro pichani kulia, wiki iliyopita
alijulikana kupitia mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya habari ambapo
anaishi maisha kuombaomba wasamaria wema
baada ya baba yake Petro Magogwa kutokuwa na uwezo kiuchumi wa kupata chakula
cha familia.
Alisema
maisha yake ni ya shida kwa familia kukosa mto wa mchana akishindia andazi moja
na maji baada ya baba yao kukosa chakula na kutokuwa na uwezo kifedha wakati
mwingine yeye na wadogo zake hutumia maparachichi kama mlo wa mchana au usiku.
Mazingira ya
mwanafunzi huyo sio ya usalama kwani
familia inaishi mbali na kijiji mpakani na nchi jirani ya Burundi nyumba yao
iliyobomoka imezungukwa na msitu kwa
maana ya miti ya parachichi, mifenezi na karatusi huku kwa majirani kukiwa na
miti ya karibea na migrevelia.
“Tuhamishwe
eneo hili na kujengewa sehemu nyingine, hapa watu wabaya wanaweza kuja na
kutuua au kutuibia ila namshukuru Mungu nikishiba nikaenda shule nataka niwe
mwalimi nakufundisha wengine”Alisema
Anthony.
|
Afisa Ustawi wa Jamii wilayani Ngara Musa Niyonsaba Balagondoza alipoutembelea Uongozi wa Shule anayosoma Anthony. |
Pia alisema
akipata chakula na kushiba hatakuwa na mawazo ya kwenda kuomba omba mpakani mwa
nchi ya Burundi eneo la Kobero na
kabanga mjini hivyo, atahuduria masomo na kuhakikisha anafuata atakachoelekezwa
na walimu hatimaye atimize malengo
kimaisha.
Afisa Ustawi
wa Jamii wilayani Ngara Musa Niyonsaba Balagondoza, ametembelea Shule ya msingi Ngundusi kubaini
mahudhurio ya Mwanafunzi Anthony na kufika kwa baba yake na kusema serikali na
jamii wakiungana mtoto huyo na ndugu zake wataboreshewa maisha.
Amesema
idara yake inasimamia na kulinda haki za watoto kwa mujibu wa sheria namba 21
ya mwaka 2009, hivyo anawashukuru wananchi walioibua mtoto huyo kwa kutumia
mitandao ya kijamii ambapo baadhi ya watu walioguswa wameanza kujitokeza
kusaidia.
Ngara, Na Shaaban Ndyamukama.
|
No comments:
Post a Comment