Mamlaka ya
Chakula na Dawa Nchini, TFDA, imezifutia usajili dawa mbalimbali za kutibu
magonjwa ya binadamu na kuziondoa kwenye soko pamoja na kusitisha matumizi yake
kutokana na kuwa na madhara makubwa kwa wagonjwa.
Hayo
yamebainishwa Jijini Arusha na Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, wakati
akifungua mafunzo ya wakufunzi wa ufuatiliaji kuhusu ufundishaji na
uhamasishaji wa masuala ya udhibiti wa madhara yatokanayo na matumizi ya dawa
zisizo salama kwa watendaji wa afya kutoka Wilaya zote za mkoa wa Arusha.
Bw. Sillo
amesema, katika kudhibiti matumizi ya dawa zisizofaa TFDA imeondoa dawa ya
Sindano aina ya Chloramphenical kwenye soko baada ya Shirika la Afya Duniani,
WHO, kubaini dawa hiyo ina madhara kwa watumiaji, Pia mamlaka hiyo imefuta
usajili wa dawa zingine kama vile Ketoconazole, pamoja na Celecoxib baada ya
kuthibitika zina madhara kwa watumiaji.
Bw.Sillo
amefafanua kwamba, lengo la mafunzo hayo ni kuongeza idadi ya wakufunzi wa
masuala ya usalama wa Dawa kutoka 73 hadi 133 na tayari katika kipindi cha
miaka mitatu TFDA imehamasisha watendaji wa afya wapatao 2,000 kote nchini .
|
No comments:
Post a Comment