Jana,November 22,2017, usiku
kulikuwa na michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya ambapo kulikuwa na michezo
nane kwenye viwanja mbalimbali barani humo.
Kwenye
mchezo uliovutia watu wengi ni ule wa Manchester United dhidi ya FC Basel
ambapo klabu hiyo ilihitaji alama moja kufuzu hatua ya 16 bora. Lakini mambo
hayakuwa hivyo kwani kunako dakika 89 vijana hao wa Basel walipata goli
lililokwamishwa ndoto za vijana wa Mourinho kusonga mbele.
Kwa sasa
Manchester United watahitaji pointi moja tu kufuzu kuingia 16 bora na endapo
Man United watapoteza mchezo wao wa mwisho dhidi ya CSKA Moscow, Klabu ya Basel
itatakiwa ishinde magoli angalau matano dhidi ya na klabu ya Benfica.
Na klabu ya
Moscow itahitaji ushindi wa goli nyingi dhidi ya Manchester United ili iweze
kujihakikishia nafasi ya kufuzu.
Timu tatu
kwenye ‘Kundi A’ yaani Manchester United, FC Basel na CSKA Moscow mpaka sasa
bado zina nafasi ya kufuzu kuingia 16 Bora ya michuano hiyo ambapo ni timu
mbili tu zinatakiwa kufuzu kwenye kila kundi.
|
No comments:
Post a Comment