Bw.Mnangagwa
ameshangaliwa na maelfu ya raia wa nchi hiyo waliofika kushuhudia mabadiliko ya
uongozini nchini humo, kufuatia kuondoka kwa Robert Mugabe madarakani baada ya
miaka 37 ya utawala wa kiimla.
Amesema kuwa
licha ya makosa yaliofanywa na Mugabe ni muhimu kukubali na kutambua mchango
wake kuhusu ujenzi wa taifa.
Amesema kuwa
mabadiliko ya umiliki wa ardhi yalifanyika na hayawezi kubadilishwa kwa kuwa
huo utakuwa ukiukaji mkubwa wa upiganiaji wa Uhuru.
Lakini rais
huo mpya ameahidi kuwalipa wakulima waliopoteza mashamba yao katika sera tata
iliotekelezwa na utawala wa rais Mugabe.
Baada ya
rais huyo mpya kuapishwa, mizinga 21 ilipigwa kumkribisha Rais Emmersonn
Mnangagwa.
Umati wa
watu ulipiga kelele kufuatia hatua ya jeshi kupiga hewani risasi 21 kama
heshima za kumkaribisha rais mpya.
|
Bw.
Mnangagwa aliapa kulinda haki za raia wa Zimbabwe.
Upinzani
unamtaka rais Mnangagwa kuwa tofauti na mtangulizi wake na kudumish ademokrasia
kwa taifa hilo lililojipatia uhuru wake mwaka 1980.
Mbali na
raia wa Zimbabwe, viongozi wengine wa Afrika wanashuhudia mabadiliko hayo
akiwemo rais wa Zambia Edgar Lungu na Ian Khama wa Bostwana.
Rais wa
zamani Zambia Keneth Kaunda na Rupia Banda nao pia wamehudhuria sherehe hizo
jijini Harare.
Emmerson
Mnangagwa ataongoza Zimbabwe kwa kipindi cha miezi nane hadi kuelekea uchaguzi
mwaka ujao, na tayari chama chake cha Zanu-PF kilimteua hivi karibuni
kupeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa urais mwaka ujao.
|
No comments:
Post a Comment