Dkt.
Louis Shika akiwa katika matukio ya upigaji picha na wahitimu wa Chuo hicho Mjini Kahama.
Bilionea
Dkt. Louis Shika ambaye amejizolea umaarufu mkubwa nchini Tanzania baada ya
kuibuka katika mnada wa kununua nyumba za mfanyabiashara Said Lugumi ametua leo
alhamisi Novemba 23, 2017 mjini Kahama kwenda kuhudhuria katika mahafali katika
chuo cha Afya cha (Kahama College of Health Science).
Dkt. Shika
akitoa hotuba kwenye sherehe za mahafali mbele ya wahitimu amesema anatambua
kuwa masomo ya sayansi hususani ya Afya karo yake ni ghali hivyo ameahidi
kuwalipia karo wanafunzi wote watakaofanya vizuri kwenye masomo yao chuoni
hapo.
“Natambua
umuhimu wa masomo ya afya na ughali wa malipo yake kwa Watanzania wenye kipato
cha chini, nitawalipia wanafunzi wote wenye uwezo darasani ambao wazazi au
walezi wao hawana uwezo wa kugharamia masomo yao.“amesema Dkt.
Shika wakati
akitoa hotuba yake kwenye mahafali chuoni hapo.
Kwa upande
mwingine Mkurugenzi wa Chuo hicho, Yona Bakungile ameeleza sababu za kumualika
Dkt. Shika katika Chuo chake kuwa ni kutokana na utaalamu wake wa masuala
ya tiba ya binadamu na umaarufu wake unaoendelea kuvuma nchini.
“Chuo
changu kinatoa mafunzo ya afya ya binadamu; licha ya umaarufu wake nchini kwa
sasa, Dk Shika ni miongoni mwa wataalamu katika fani ya utabibu ndiyo maana
nimemwalika.
Naamini atawashauri na kuwapa hamasa wahitimu na wanafunzi
wanaoendelea,” amesema Bakungile kwenye mahojiano yake na gazeti la
Mwananchi.
Tazama picha
za Dkt. Shika akiwa na wadau mbalimbali chuoni hapo (Picha na Mtandao).
|
No comments:
Post a Comment